JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wakenya wamaliza msitu Tanga

*Maofisa wahusika wawakingia kifua

Hifadhi ya Msitu wa Mtae wenye ukubwa wa hekta 3,182 katika Tarafa ya Maramba, wilayani Mkinga, Tanga, iko hatarini kutoweka kutokana na uvamizi unaofanywa na raia wa Kenya, kwa baraka za baadhi ya viongozi na wananchi wa Tanzania.

WARAKA WA MIHARE

Waraka wa Mihale kwa Watanzania

Amani iwe kwenu wapenzi wasomaji wa Gazeti la JAMHURI. Karibuni katika safu mpya ya ‘Waraka wa Mihale kwa Watanzania’ itakayokuwa ikijadili mambo mbalimbali yahusuyo mustakabali wa nchi yetu.

Yah: Eti serikali tatu, hiyo moja tu matatizo

Wanangu, nianze kwa kuwashukuru kwa kuwa pamoja katika kipindi hiki cha mchakato wa katiba mpya ya nchi yetu. Naiita katiba mpya kwa kuwa hatujawahi kuifuta tuliyonayo sasa isipokuwa tulikuwa tunaijazia viraka vya hapa na pale ili kufukia mashimo.

Mtuhumiwa Malele anaweza kuishitaki Polisi

 

. Ni kwa kumtangaza mgonjwa wa akili

Kijana aliyejitangaza kung’atuka ushirika wa mtandao uliohusika kumuua aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, anaweza kulishitaki jeshi hilo kwa kumtangaza kuwa ni mgonjwa wa akili.

RASIMU YA KATIBA YA TANZANIA 2013

Hofu yatanda Z’bar

*Walio Tanganyika kugeuka wawekezaji

*Wasiwasi watanda, wanunua ardhi Bara

*Wahoji Tume ya Warioba kufuta Takukuru

Mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ya kuondoa suala la ardhi katika mambo ya Muungano, yamezaa hofu kwa Wazanzibari wanaoishi Tanzania Bara na ndugu zao walioko Zanzibar.

….Makundi ya urais yayeyuka

Rasimu ya Katiba Mpya imeyanyong’onyeza makundi ya wanaowania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa muda mrefu kumekuwapo mjadala mkali wa nani anayestahili kuwania kiti hicho, lakini mbio hizo zimepunguzwa kasi na umaarufu wake, baada ya rasimu kupendekeza kuwapo kwa muundo wa Serikali Tatu – Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na Tanzania Bara (Tanganyika).