JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Siku za Ekelege TBS zahesabika

Wakati wowote kuanzia sasa Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) aliyesimamishwa kazi mwaka mmoja uliopita, Charles Ekelege atapandishwa kizimbani kujibu tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya ofisi.

Yah: Tuliangalie sakata la elimu kwa sasa [2]

Wiki jana nilizungumzia juu ya elimu ya kambo wakati nikihitimisha barua yangu. Nilijaribu kuangalia tofauti za elimu ya sasa na ya zamani japokuwa hazipaswi kufananishwa kutokana na mitaala na manufaa baada ya masomo. Sisi tulifundishwa kujitambua na kujitegemea na ninyi kwa sasa mnafundishwa kutegemea na kutojitambua.

KAULI ZA WASOMAJI

Polisi iwakamate waliomuua Barlow

Ili Jeshi la Polisi liweze kujijengea hesima katika jamii, lioneshe makali yake katika kushughulikia mtandao wa mauaji ya RPC Liberatus Barlow, kufuatia maelezo yaliyotolewa na Malele.

Boniface Nyerere, Dar

RIPOTI MAALUMU

IGP Mwema ampa hifadhi ‘muuaji’ wa Barlow

*Apewa ulinzi wa polisi wenye silaha

*Anapewa huduma zote za kibinadamu

*Mbunge, Naibu Waziri wahusishwa ujangili

Kijana Mohamed Malele aliyejisalimisha kwenye vyombo vya ulinzi na usalama akijitambulisha kuwa mshirika wa mtandao uliohusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, amepewa ulinzi maalumu.

Bila uwajibikaji Tanzania tutakwama (1)

Baada ya kusoma mengi katika magazeti na kuona kwenye runinga namna lile jengo la ghorofa 16 lilivyoporomoka, mimi, huenda na wengine wengi. tumeingiwa na wasiwasi.

FASIHI FASAHA

Watanzania tunakinyanyasa,

tunakibeua Kiswahili – 7

Sina budi kutoa shukrani kwa wale wote walioniunga mkono katika mada hii ya Watanzania tunakinyanyasa na kukibeua Kiswahili. Ni dhahiri Watanzania wanatambua na wanajali lugha yao ya Kiswahili. Asante. Baadhi ya Waswahili wanasema kuwa lugha ya kaya, kabila, rika, masikani na vijiweni, na hata sehemu zetu za kazi, au michezo zisiwe ni vigezo kuwa Watanzania hawakithamini Kiswahili. Hizo ni lugha za msimu tu.