JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Nchi imetafunwa!

*Hazina yatumia Shilingi bilioni 8, taasisi za umma

zachangishwa, ‘wajanja’ watafuna mamilioni

*Vifaa vya Obama vyaokoa jahazi, sare, mikoba, vyagharimu

mil. 400/-, vinyago navyo balaa!

*Karamu, chupa za kahawa, miavuli mil. 390/-,

Burudani ya muziki yatafuna milioni 195/-

*Dewji agoma kuchangia, Katibu Mkuu Haule

arushiwa kombora, yeye ajitetea

Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), uliomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, umeigharimu Serikali Sh bilioni nane.

Sakata la Iddi Simba bado bichi

*Ikulu, ofisi ya CAG washangazwa kuachiwa

*Uamuzi uliofanywa na DPP wazua maswali

Kuachiwa kwa mwanasiasa Iddi Simba, ambaye hivi karibuni alikuwa akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kabla ya Mkurugenzi wa Mshitaka nchini (DPP), kuamuru awe huru, kumeibua mgongano mkubwa serikalini.

Waraka kutoka mtandaoni

Wanaosoma Ujerumani wamlilia Kikwete

Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, kwanza naomba niombe msamaha kwa kutumia forum hii badala ya kukuandikia binafsi. Hii ni kwa sababu ya dharura ya jambo lenyewe linalohitaji hakika hatua za haraka sana ili kuokoa haya yanayotokea. Hivyo, naomba unisamehe kwa kuweka bayana hili hapa.

Hongera Kikwete, Membe; Salva rekebisha kasoro hii

 

Julai 1 na 2 zilikuwa siku za pekee katika historia ya Tanzania. Tanzania ilihitimisha kilele cha ugeni mkubwa kuja hapa nchini ndani ya mwaka mmoja. Katika siku hizi taifa lilikuwa na ugeni mkubwa wa Rais wa Marekani, Barack Obama.

 

Afrika inaelekea kutawala uchumi Afrika (1)

 

Nawasalimu wasomaji wote, ninawapongeza na kuwashukuru wote ambao wamekuwa wakiwasiliana nami. Mbarikiwe. Itakumbukwa kuwa huko nyuma nimepata kuandika makala iliyokuwa na kichwa, ‘Naiona Afrika ikiinuka tena’.

 

Obama ampandisha chati Lowassa

Hatua ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion Ubungo jijini Dar es Salaam, imeamsha mjadala mzito katika jamii uliowafanya Watanzania kuanza kumhurumia Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wakiona alionewa.