JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Katiba ya Simba inavyompa Rage kifua

Kabla ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya Dar es Salaam siku kadhaa zilizopita, baadhi ya wanachama wa klabu hiyo walitaka kuwapo agenda ya kufanya marekebisho katika baadhi ya vipengele vya katiba ya Wekundu hao wa Mtaa wa Msimbazi.

Ulaji wa mpya waibuliwa

*Malipo ya ndege utata mtupu

*Wahusika wakalia kuti kavu

*Waziri Membe aingilia kati

 

Kukiwa na taarifa kwamba uongozi wa juu serikalini umeagiza kuchunguza ulaji wa mamilioni ya shilingi wakati wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), siri nzito za ufisadi zimeendelea kuanikwa.

Yah: Nimechoka na nyimbo zenu sasa

Pamoja na kwamba natukanwa sana na vijana wa dotcom, wakiamini kuwa wako sahihi kwa matusi yao na uhusiano wa kile ambacho nakizungumzia au kukiandika katika waraka huu, najua iko siku nao watakuwa BBC, yaani ‘Born Before Computer’ kwa kizazi chao kitakachokuwa kimekengeuka kuliko wao.

UNESCO, WHC wakubali barabara NCAA-SENAPA

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kituo cha Urithi wa Dunia (WHC) wameikubalia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ifanye upembuzi yakinifu wa barabara ya Lodoare-Serengeti.

Mzungu afanyiwa tohara ya kimila Afrika Kusini

Kijana wa kiume Mzungu mwenye asili ya Afrika Kusini, amefanyiwa tohara ya kimila nchini humo. Tohara ya kimila katika baadhi ya makabila nchini Afrika Kusini huashiria hatua ya ukuaji kwa kijana inayompatia hadhi ya kuitwa mtu mzima katika familia.

Soka la Tanzania bado lina changamoto

Wakati  timu ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ilipopoteza mchezo wake dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wiki iliyopita kwa kufungwa goli 1-0, wadau wa soka walikuwa na mengi ya kusema dhidi ya kipigo hicho.