JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Yah: Tanzania na maendeleo ya mdomo

Nianze kwa kuwashukuru sana wazazi wangu walionikanya wakati naoa kwamba maisha ya ndoa ni kama glasi ndani ya kabati, ipo siku lazima kabati litayumba na glasi zitagongana, na ikitokea hivyo katika maisha yangu ya ndoa lazima nitumie kuta nne za chumbani kwangu kumaliza kelele zetu za glasi, ugomvi na sintofahamu yoyote ile.

Mkombozi wako kiuchumi ni wewe

 

Wiki iliyopita niliandika makala kuhusu fikra zinavyoweza kukukomboa kiuchumi. Katika makala yale nilieleza kuwa ili kufanikiwa kibiashara na kiajira tunahitaji hamasa kuliko hata kubadilisha siasa zinazotawala na Katiba mpya. Nilisema mtu namba moja wa kuukomboa uchumi wako ni wewe mwenyewe.

 

Extra Bongo wajipanga kutumbuiza Idd

Bendi ya Muziki wa dansi ya Extra Bongo ya jijini Dar es Salaam inajipanga kuhakikisha inafanya maonesho ya kusisimua wakati wa kusherehekea Sikukuu ya Idd.

Lady Gaga kutumbuiza MTV

Msanii  maarufu  wa muziki wa Pop, Lady Gaga, anatarajiwa kutumbuiza katika tuzo za muziki za MTV zitakazofanyika Agosti, mwaka huu. Litakuwa onesho lake la kwanza baada ya kufanyiwa upasuaji wa sehemu za nyonga.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Tusipuuze misingi ya ujamaa

“Kama chama chetu kitapuuza misingi ya ujamaa, basi kitakuwa kinapuuza msingi mmoja muhimu wa amani na utulivu katika taifa hili. Tutavuruga amani maana tutakuwa tumeondoa matumaini ya kuleta maendeleo yanayoheshimu utu na usawa.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarange Nyerere.

Kocha URA: Yanga ni bora kuliko Simba

Hivi karibuni timu ya soka inayomilikiwa na Mamlaka ya Mapato ya Uganda (URA), ilitua hapa Tanzania kucheza mechi kadhaa za majaribio.