JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kodi ya simu inarejesha ‘Kodi ya Kichwa’

Taifa letu lipo katika mtikisiko mkubwa. Kuna mjadala mkubwa unaoendelea juu ya uanzishwaji wa kodi ya kumiliki simu. Kodi hii inatajwa na wengi kuwa ni kama kodi ya ‘Kichwa’ iliyobatizwa jina la kodi ya maendeleo baada ya Uhuru.

Funga ya Ramadhani, hukumu, fadhila, adabu zake – 3

Katika sehemu ya pili ya makala haya, Sheikh Dk. Ibrahim Ghulaam, alizungumzia nyudhuru za funga, nguzo za funga, unavyothibiti kuingia Mwezi wa Ramadhani na yanayobatilisha funga. Sasa mfuatilie zaidi katika sehemu hii ya tatu…

Tanzania imefikia kilele katika dawa za kulevya

Dawa za kulevya zinazidi kuchafua jina la Tanzania. Zimekuwapo taarifa za orodha ya watu wanaotumia au kuuza dawa hizo hapa nchini, lakini kadri siku zinavyopita tatizo linazidi kuwa kubwa kwa kiwango cha kutisha. Katika hali isiyo ya kawaida, Mtanzania aliyeko kifungoni nchini China ameamua kuanika ukweli wa kinachoendelea Tanzania.

Kesho nataka kuwaamini polisi, nani anipe mwongozo?

Sitaki iwe mbali, bali mapema sana kesho asubuhi nataka nitii bilakushurutushwa na mtu yoyote maana wengine wameishasema kuwa wamechoka na mchoko wao wameishauhalalisha kwa kupitisha amri, amri ambayo mahakama imethibitisha kuwa ilikuwa amri ya iliyopungukiwa vigezo kutoka kwa mtoto wa mkulima.

Rais JK, orodha ya mapapa wa mihadarati imeyeyukia wapi?

Katika gazeti hili kuna barua iliyoandikwa na mmoja wa Watanzania walio kwenye magereza Hong Kong, kutokana na usafirishaji mihadarati.

Maghoba: Tanzania isipuuze vitisho vya Kagame

Mwanajeshi mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Frank Maghoba, ameitahadharisha Tanzania, akiitaka kutopuuza kauli ya vitisho inayodaiwa kutolewa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, dhidi ya Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete.