JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Katiba Mpya iakisi uzalendo (Hitimisho)

Sehemu iliyopita, mwandishi alinukuu ibara ile ya kwanza ya

Mkataba wa Muungano na kusema mtu akiisoma atajua ilikuwa na viashiria vya undugu na umoja wetu wa asili kati ya watu wa nchi hizi mbili – Tanganyika na Zanzibar. Hii ni sehemu ya mwisho ya mfululizo wa makala ya Katiba Mpya iakisi uzalendo. Endelea

Maneno mazito namna hii na ya kizalendo kutoka kwa watu wa Zanzibar, leo mtu aje aseme mbona hatukushauriwa: Oh! mbona hatukuulizwa hivi. Wanaofyatuka kusema hivi walikuwa na umri gani Aprili 24, 1964? Pengine wala hawakuwa wameingia ulimwenguni. Leo waje na stori za watu wa Zanzibar eti waulizwe wanautaka Muungano au hawautaki ndipo Katiba yetu iandikwe ni sahihi kweli wazee wenzangu?

MISITU & MAZINGIRA

Misitu inavyokinufaisha Kijiji cha Nanjilinji ‘A’ (1)

Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi ni mojawapo za wilaya chache Tanzania Bara zilizobahatika kuwa na misitu ya asili ya kutosha ikilinganishwa na maeneo mengine nchini. Pamoja na kuwa na rsilimali misitu ya kutosha yenye aina za miti ya thamani sana mfano, mipingo (Dulbergia melanoxylon), Kilwa ni kati ya wilaya maskini nchini.

KONA YA AFYA

 

Vidonda vya tumbo na hatari zake (7)

Kuchelewa sana kula: Kuna maelekezo mengi ya wataalamu juu ya muda mzuri wa kula. Kuchelewa sana kula huweza kuleta tatizo la kiafya ikiwa ni pamoja na vidonda vya tumbo kama mtu atakuwa tayari ana mwelekeo wa kupata vidonda. Vile vile kula wakati husikii njaa si jambo zuri kwa afya. Kula ukiwa huna njaa (au umeshiba) hudhoofisha utendaji kazi wa mifumo inayohusika na usagaji chakula.

 

Mpunga, mahindi, miwa kuikomboa Tanzania

Leo nataka kujikita katika suala la Majadiliano ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote Smart Partnership Dialogue, ambayo ni dhana ya kiubunifu na msingi wake ni kanuni ya ‘Stawi Jirani Yangu kwa Manufaa Yetu Sote’.

Maghoba: Tanzania isipuuze vitisho vya Kagame – Hitimisho

Wiki iliyopita, sehemu ya kwanza ya makala haya pamoja na mambo mengine, mwanajeshi na mbunge mstaafu, Frank Maghoba, alieleza mtazamo wake kutokana na kauli ya vitisho inayodaiwa kutolewa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame dhidi ya Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete. Sasa endelea na sehemu hii ya mwisho…

Chanzo cha msuguano

Inaelezwa kuwa msuguano huo baina ya Rwanda na Tanzania ulianza kujitokeza siku chache baada ya kumalizika kwa kikao cha viongozi wa Nchi za Maziwa Makuu, kilichohudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, chini ya uenyekiti wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Sitta aache kumchafua Edward Lowassa

Siku zote napenda kufuatilia siasa za Tanzania. Ni siasa hizi za kuchafuana. Siasa za kuchafuana si ngeni katika jamii yetu. Mtu akimwona mwenzake kazidi kwa jambo jema katika jambo fulani, basi atamchafua ili jina lake lionekane kuwa si kitu.