JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wauza ‘unga’ waanza kutajwa

Wakati Watanzania wengi wakiwa wameamua kuwaanika hadharani nguli wa biashara ya dawa za kulevya, Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo, naye amepasua ukweli wa mambo akisema hali inatisha.

Watu 10,262 wakacha ARVs

 

Watu 10,262 wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi mkoani Mwanza, hawajulikani waliko kwa zaidi ya miezi mitatu sasa baada ya kutohudhuria kliniki ya kutoa dawa hizo.

Jeshi la ‘bodaboda’ latembeza mkong’oto wilayani Geita

Jeshi lisilo rasmi la vijana zaidi ya 60 wanaofanya kazi ya kubeba abiria kwa kutumia pikipiki (bodaboda), huku wakiimba kibwagizo cha ‘wapigwe tu’, wameteka mtaa na kutembeza kipigo kikali kwa abiria wao mmoja.

MAUAJI YA BARLOW

 

Malele aendelea kuteseka Muhimbili

Maendeleo ya matibabu ya Mohamed Malele aliyetangaza siri za mtandao unaodaiwa kuhusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, ni kitendawili.

Tutelekeze wabunge, tuwawezeshe polisi

Wiki hii nimewaza na kuwazua. Kwa furaha nimepokea mrejesho kutoka kwenu wasomaji wangu. Hakika nimefurahi jinsi mlivyolikubali gazeti JAMHURI, na jinsi mawazo tunayoyatoa mnavyoyaunga mkono. Nasema asanteni sana na mkihisi tumekosea, msisite kutusahihisha.

Funga ya Ramadhani, hukumu, fadhila, adabu zake (Hitimisho)

Sheikh Dk. Ibrahim Ghulaam, katika sehemu ya tatu ya makala

haya alielezea kwa kina kuhusu yasiyofunguza na adabu za funga. Sasa fuatana naye katika sehemu hii ya mwisho…

Fadhila za funga

Zimepokewa hadithi nyingi zinazoelezea fadhila za funga ya Ramadhani, miongoni mwa hizo ni zifuatazo: