JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Tarime wataja kinachowalazimu kukodisha ardhi kwa Wakenya

Wananchi wa Kata ya Bumera, Wilaya ya Tarime mkoani Mara, wametaja sababu mbalimbali zinazofanya kuwapo kwa wimbi kubwa la ukodishaji wa mashamba, kwa ajili ya kulima zao haramu la bangi kwa raia wa Kenya.

Ansar Sunni: Hatumtambui Sheikh Ponda

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu wa Ansar Sunni, Sheikh Salim Abdulrahim Barahiyan, amesema jumuiya hiyo haina uhusiano na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Waislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda. “Mimi sijawahi kukaa na Sheikh Ponda katika kikao hata kimoja. Tuna misikiti karibu 20 Tanga, hajawahi kuingia hata msikiti mmoja,” amesema Sheikh Barahiyan.

Barua ya wazi kwa Waziri Mwakyembe

Mheshimiwa Waziri Dk. Harrison Mwakyembe, tunayo heshima kuchukua nafasi hii kukujulisha kuwa matrekta haya unayoyaona yamekwishalima sana na sasa hayawezi kazi hiyo tena. Ukiyafukuza mjini ni wazi hayatakwenda kulima, maana mengi hayana uwezo tena wa kufanya kazi hiyo.

FASIHI FASAHA

Tusizikwe tungali hai -1

Tusizikwe tungali hai. Nimeanza na kaulimbiu hiyo iliyobuniwa na kutumiwa na wastaafu wa iliyokuwa Radio Tanzania Dar es Salaam-(RTD)  sasa TBC.

Wauza unga 250 nchini watajwa

*Soma orodha uone maajabu, wamo masheikh, wachungaji

*Wengi wanatoka Dar es Salaam, Tanga, Zanzibar, Morogoro

*Mahakama yawaweka chini ya uangalizi, wanaripoti polisi

Majina ya Watanzania 255 wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya yamejulikana, na JAMHURI imeamua kuyachapisha. Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa kwenye orodha hiyo wamo watu maarufu na baadhi wamekuwa wakitoa misaada, huku wengine wakijifanya ni wazee wa kanisa na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

Tujisahihishe: Mwalimu Nyerere

 

UMOJA wa kundi lolote ni sawa sawa na umoja wa viungo mbalimbali vya mwili au mtambo. Viungo vya mwili havina budi vitii kanuni zinazoviwezesha kufanya kazi yake sawa sawa. Lakini haviwezi kutii kanuni hizo kama haviko katika hali ya afya njema. Mara kiungo kimoja kinapokuwa hakina afya safi, huanza kuvunja kanuni za kazi na mwili mzima hupata taabu.