JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wauza unga 250 nchini watajwa

*Soma orodha uone maajabu, wamo masheikh, wachungaji

*Wengi wanatoka Dar es Salaam, Tanga, Zanzibar, Morogoro

*Mahakama yawaweka chini ya uangalizi, wanaripoti polisi

Majina ya Watanzania 255 wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya yamejulikana, na JAMHURI imeamua kuyachapisha. Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa kwenye orodha hiyo wamo watu maarufu na baadhi wamekuwa wakitoa misaada, huku wengine wakijifanya ni wazee wa kanisa na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

Tujisahihishe: Mwalimu Nyerere

 

UMOJA wa kundi lolote ni sawa sawa na umoja wa viungo mbalimbali vya mwili au mtambo. Viungo vya mwili havina budi vitii kanuni zinazoviwezesha kufanya kazi yake sawa sawa. Lakini haviwezi kutii kanuni hizo kama haviko katika hali ya afya njema. Mara kiungo kimoja kinapokuwa hakina afya safi, huanza kuvunja kanuni za kazi na mwili mzima hupata taabu.

KAULI ZA WASOMAJI

Wanahabari tembeleeni pia vijijini

Waandishi wa habari jaribuni kutembelea pia na maeneo ya vijijini kwa sababu huko kuna matukio mengi ya kutisha na kusikitisha, lakini vyombo vya habari vimekuwa havielekezi nguvu kubwa vijijini kama vinavyofanya maeneo ya mijini.

Obe Mlemi, Mugumu – Serengeti

0768 235 817

Pikipiki zinatumaliza, DPP futa aibu hii

Kwa muda sasa  yamekuwapo maelezo ya kuonesha jinsi pikipiki zilivyo janga la kitaifa. Pikipiki zimekuwa zikishutumiwa kwa kusababisha ajali, kupoteza nguvu kazi na kuongeza idadi ya walemavu au vifo kwa kasi ya ajabu hapa nchini.

Ukitaka mafanikio halisi lipa kodi kwa uaminifu

Kwa hivi sasa mashine za kielektroniki za EFD za TRA, imekuwa ndiyo habari ya ‘mjini’ kwa wafanyabiashara karibu kila kona nchini. Hii imekuja baada ya awamu nyingine ya TRA kujumuisha wafanyabiashara wengi zaidi tofauti na ilivyokuwa mwanzo wakati zikiingia.

Siri za Ponda kupigwa risasi zavuja

Siri nzito zimevuja juu ya sababu za Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda kupigwa risasi mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Wakati Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, akiliambia gazeti la Daily Telegraph la Uingereza Jumamosi usiku kuwa polisi ndio waliompiga risasi Ponda wakati anajaribu kukimbia, magazeti ya Tanzania Shilogile ameyaambia hajui kilichotokea.