JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wakala wa Kaseja kutimuliwa nchini

* Ni yule wa FC Lupopo

Kuna kila dalili kuwa safari ya usajili wa golikipa wa namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Juma Kaseja, kujiunga na timu ya soka ya FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kukayeyuka, kufuatia taarifa kuwa huenda wakala wake, Ismail Balanga Bandua, akatimuliwa nchini muda wowote.

JAMHURI YA WAUNGWANA

 

Kwa mwaka Mtanzania hafanyi kazi kwa siku 140!

Makala yangu ya wiki iliyopita ya “Wakati mwingine Wakristo wanaanzisha chokochoko”, imepokewa kwa hisia tofauti na wasomaji wa safu hii.

Makala ililenga kupinga msimamo wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) wa kutaka Jumapili isitumike kwa kura ya maoni inayotarajiwa kupigwa kama sehemu ya kupata Katiba mpya.

 

Mapambano dhidi ya wauza ‘unga’ ni mzaha mtupu

Nazungumzia Serikali inayoendesha mapambano dhidi ya dawa za kulevya. Nionavyo mimi ni mzaha mtupu. Ni sawa na kukumbuka kujifunika shuka wakati kumeshakucha.

FIKRA YA HEKIMA

Kilio cha wafanyakazi wa OSHA kisipuuzwe

Dalili mbaya zinanyemelea Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA). Kuna hatari ya ofisi hiyo kutokalika ikiwa mamlaka za juu zitaendelea kupuuza malalamiko ya wafanyakazi dhidi ya Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo ya serikali.

Kabantega: Mzalendo anayekabiliwa na kifo kama Dk. Masau

*Ni bingwa wa kutengeneza test tube aliyetelekezwa

*Miaka 27 sasa anapigwa danadana na wakubwa serikalini

*Mitambo, malighafi alivyozawadiwa vinaozea bandarini

*Mwalimu Nyerere, Rais Kikwete, Lowassa walimkubali

*Umoja wa Mataifa, AU, Sudan Kusini, Rwanda wanamlilia

Mwaka 2009 nilikutana na Mtanzania aliyenivutia kwa ubunifu, uwezo wake wa kiakili, na zaidi ya yote ni uzalendo wake kwa nchi yake. Nikamwomba na yeye akakubali kufanya mahojiano. Lengo lilikuwa kuwawezesha Watanzania, hasa watu wenye mamlaka ya uongozi waweze kumtambua, kumsaidia na kumtumia ili ndoto yake itimie.

CECILIA PETER: Mwanamke dereva jasiri wa bodaboda

* Akerwa na watekaji, waporaji wa pikipiki

Ni saa 11 jioni nawasili katika Kituo cha daladala cha Kibamba, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Ni umbali wa kilometa 30 kutoka katikati ya jiji hili. Hapa nakutana na mwanamke anayeitwa Cecelia Peter. Ninagundua haraka haraka kuwa mama huyu ni maarufu katika eneo hili na maeneo jirani.