JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kamala asisitisa uzalishaji almasi

Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dk. Diodorus Kamala, ameomba Kampuni ya Petra Diamonds ya nchini humo kuongeza uzalishaji na ubora wa almasi inayozalishwa hapa Tanzania.

Tanzania iwe kwa Watanzania kwanza

Chama cha Tanganyika African National Union (TANU) kilichodai Uhuru wa nchi hii kilikuwa na ahadi nzuri. Baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilizirithi.

Matatizo ya sekta ya vitabu Tanzania

Kama tujuavyo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeanza kutekeleza mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), huku Taifa likiwa na matatizo makubwa ya kuwapo kwa vitabu vibovu shuleni. Ni matatizo yaliyotokana na sera mbovu ya vitabu Tanzania.

Kumbe ndio maana trafiki wanachukiwa

 

Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikisikia na kuona jinsi wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya nchi hii, wanavyowalalamikia askari polisi wa kitengo cha usalama barabarani (trafiki). Siyo siri ndugu zetu hao wanachukiwa na wananchi wengi.

Vidonda vya tumbo na hatari zake (13)

Katika toleo la 12 la mfululizo wa makala haya, Dk. Khamis Zephania alieleza dalili za tumbo kujaa gesi na tatizo la kufunga choo. Sasa endelea kumfuatilia katika sehemu hii ya 13.

Kesi kubwa ya ‘unga’ yatajwa Dar

*Ni ya Mama Lela aliyetajwa na Rais Obama

Kesi ya mtuhumiwa mkubwa wa dawa za kulevya duniani aliyekamatwa eneo la Mbezi jijini Dar es Salaam imetajwa wiki hii.

JAMHURI ilipata taarifa kutoka Mahakama Kuu kuwa kesi hii, inahusisha watuhumiwa wanane akiwamo Mtanzania Mwanaidi R. Mfundo. Pia nchini Kenya na Marekani anafahamika kwa jina la Naima Mohamed Nyakiniywa au Naima Nyakinywa, maarufu Mama Lela huko Mbezi, jijini Dar es Salaam akiwa pamoja na Wakenya saba, imetajwa jana Mahakama Kuu.