JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Kwa mtego huu wa UKAWA hautamnasa Rais Kikwete

Tukio la hivi karibuni ambapo wajumbe wanaounda kundi la Umoja wa Katiba wa Wananchi (UKAWA) kuamua kuyakana makubaliano yaliyofikiwa baina yao na Rais Kikwete kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), haliwezi kupita bila kuhojiwa.

‘Utatu wa Maliasili’ ni wa ulaji

Watanzania tuna ugonjwa mmoja mbaya sana. Ugonjwa wa kutokuhoji lolote. Hatuna utamaduni wa kuhoji vitendo na kauli tata za viongozi na watawala wetu. Tumeridhika kuwa liwe liwalo; au yote maisha.

Kutokana na hali hiyo hatuna na hatuoni sababu za kuwawajibisha viongozi waongo, wazushi, matapeli na mafisadi. Matokeo yake viongozi na watawala hawa wamekuwa wakitumia udhaifu wetu wa kutokuhoji kufanya watakavyo.

Mbowe moto

.Adai moto aliowasha hauzimiki mpaka kieleweke 2015

.Asema anaumizwa kuteketea mamilioni Bunge la Katiba

.Atamba ipo siku polisi watazitambua haki za Watanzania

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema anashangazwa na vigogo wa Jeshi la Polisi kufanya hila za kumkabili, ilhali wanaona namna Watanzania walivyodhulumiwa haki yao kupitia Bunge Maalum la Katiba.

Rais nje ya nchi kwa nusu mwezi!

Wiki iliyopita nilikuwa mkoani Mara. Nilifika katika Kijiji cha Sabasaba wilayani Butiama, mahali ambako roho takribani 40 za Watanzania zilipotea katika ajali iliyohusisha magari matatu — mawili yakiwa mabasi ya abiria yanayofanya safari zake kati ya miji ya Sirari, Musoma na Mwanza.

Sababu za Italia kusuasua kiuchumi

Licha ya dunia kuwa na jumuiya nyingi za kisiasa na kiuchumi, Umoja wa Ulaya (EU) ni kati ya jumuiya za kisiasa na kiuchumi zilizofanikiwa kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na jumuia nyingine duniani.

Ni jumuiya inayounganisha watu zaidi ya milioni 500 kutoka mataifa wanachama ishirini na nane huku pato la jumuiya likitajwa kufikia dola trilioni 18.45.

Tanzania ijitoe Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Bila shaka sisi sote tunajua kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Umoja wa Nchi za Afrika Mashariki unaojumuisha nchi tano za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Tanzania.

Watu husema ‘umoja ni nguvu’ kwa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni umoja, basi watu wanalazimika kumshangaa mtu anayewahimiza wenzake wajitoe kwenye umoja. Ni kweli umoja ni nguvu. Lakini inategemea unafanya umoja na mtu wa aina gani. Hii ni kusema kwamba wakati mwingine umoja ni udhaifu na unaweza kumletea mtu madhara makubwa.