JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

MAGHALA TANDAHIMBA: Vigogo wamfuata Waziri Chiza

Kampuni ya Tandahimba Quality Control System, iliyoshinda kwa utata zabuni ya kuendesha maghala ya Muungano wa Vyama vya Ushirika Wilaya za Tandahimba na Newala (TANECU), inahaha ngazi za juu ili ikabidhiwe maghala hayo.

Kampuni hiyo inatafuta njia za mkato, ikiwezekana kwa kumtumia Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, ili ikabidhiwe shughuli hiyo yenye ukwasi mkubwa.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Leseni za Maghala, Fidelis Temu, ameiandikia Tandahimba Quality Control System barua ili ijibu hoja za pingamizi zilizotolewa na wadau kadhaa kwa maandishi.

Al-Shaabab, Boko Haram waungana

KUNDI la kigaidi la Al-Shabaab la nchini Somalia ko kwenye wakati mgumu kama Boko Haram la Nigeria ambalo taarifa za kuuawa kwa kiongozi wake, Abubakar Shekau.

Kutokana na hali hiyo, taarifa zinasema kwamba kumekuwa na mawasiliano baina ya makundi ya kigaidi kuunganisha nguvu za pamoja ili kukabiliana na hali ya kuzidiwa na wapinzani wao katika harakati zao.

JK amchoka Nyalandu

*Atinga Marekani na msanii wa ‘Bongo Movie’

*Wabunge wamsubiri kumsulubu Novemba

*Safari, hoteli ghali zatafuna mamilioni ya shilingi

*Ofisi zake za wizarani ‘zakaribia kuota majani’

 

Na Mwandishi Wetu

 

Rais Jakaya Kikwete ameanza kuchoshwa na vituko vya Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, JAMHURI limethibitishiwa.

Malengo ya kazi (2)

Lazima wahakikishe kwamba kazi zote zinaendeshwa barabara, na pamba ya aina itakiwayo inapatikana na wakati ule ule inapoatakiwa; wahakikishe kwamba hakuna kipingamizi  kutoka hatua moja hata nyingine; kwamba kuna uhusiano baina ya kazi mbalimbali, na kwa sababu hiyo hakuna mfanyakazi anayekaa bure kungojea mwenzake amalize kazi yake.

Wakubwa wa kazi hawana budi kuhakikisha kwamba wananunua pamba ya kutosha, na kwamba wana mahali pa kuuzia nguo  zinazotengezwa; kwamba mishahara inalipwa bila ya kuchelewa;  kwamba hesabu ya fedha zinazowekwa sawa sawa; kwamba mitambo inakaguliwa ipasavyo; na mambo mengine kadha.

Wataalamu: Mtoto mpotevu Dar ana tatizo la kisaikolojia

Wanataaluma nchini wamesema kwamba wamefuatilia habari za kupotea na kupatikana kwa mtoto Happy Rioba (9), na kwa haraka wamegundua kwamba binti huyo ana tatizo la saikolojia tofauti na wengi wanaohusisha ushirikina.

Happy, anayeishi na mama yake, Sarah Zefania huko Mkuranga mkoani Pwani, aliripotiwa na vyombo vya habari kupotea na kupatikana zaidi ya mara moja, tukio lililovuta hisia za watu wengi.

Tugeukie mabadiliko ya Katiba, maandamano tuwe macho

 

Kumbukumbu zinanionesha sasa kuwa Watanzania wengi wanaamini kuwa suala la Katiba Mpya haliwezekani tena chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Ametafuta pa kutokea na kuamua kuelewana na wapinzani kupitia Kituo cha Demokrasia (TCD) na wakubwa hawa wakakubaliana yafanyike mabadiliko ya 15 ya Katiba.