JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Wanaoiponda UDA wamekosa uzalendo

Tumetafakari kwa kina juu ya taarifa zinazolaumu “Serikali kubariki ufisadi wa UDA.” Lawama hizo hutolewa na Watanzania wachache sana wanaopinga Kampuni ya wazawa ya Simon Group kuuziwa hisa za UDA.

Hoja za msingi malalamiko hayo ni kwamba Simon Group haikufuata taratibu na sheria, na pia kwamba haikuzingatia thamani halisi ya shirika hilo. Tunachofahamu sisi kwa sasa ni kwamba uuzwaji huo uko sahihi na hakuna kinachoweza kubadilika, kwani taratibu na sheria zote zilizingatiwa kikamilifu wakati wa uuzaji wa hisa za UDA kwa Simon Group.  

Wamiliki mabasi wana wajibu wa kupunguza ajali

Tatizo la ajali za barabarani limekuwa ni moja ya changamoto kubwa sana katika sekta ya usafiri wa barabara hapa nchini. Katika kipindi cha mwanzo wa mwezi Septemba, 2014 kumetokea ajali za barabarni kubwa zaidi ya mbili katika mikoa ya Mara na Tabora, ambako watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.

Ninachokumbuka kuhusu mradi wa maji Ziwa Victoria

Katika dunia kuna mambo yakitokea unajiuliza kwa nini yametokea. Unajiuliza ni hivi hivi au kuna msukumo, ila yote kwa yote nimejiwekea utaratibu wa kusimamia ukweli. Mara zote naamini ukweli unamweka mwanadamu huru, na hapa leo kama nifanyavyo siku zote nitajaribu kueleza ukweli ninaoufahamu.

Ukweli kuhusu elimu ya Lembeli

Mwalimu Julius Nyerere, ambaye Mheshimiwa James Lembeli amewahi kujifananisha naye, aliwahi kusema kuwa ikitokea mtu wa kawaida akampiga mkewe hadharani, hii haiwezi kuwashughulisha watu na wala haiwezi kuwa habari. Lakini ikatokea yeye (Mwalimu) akafanya hivyo, basi hiyo itakuwa habari kubwa mno.

Mwalimu Nyerere na mgombea binafsi

Mei Mosi, 1995 Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akiwa mgeni rasmi kwenye Sherehe za Mei Mosi mjini Mbeya, alizungumza mambo mengi yaliyolihusu Taifa. Miongoni mwa mambo hayo ni haki ya kuwapo mgombea binafsi. Rasimu ya Katiba Mpya (ya Jaji Warioba) ilizingatia jambo hili muhimu. Hata hivyo, Bunge Maalum la Katiba (katika Rasimu ya Samuel Sitta) limeminya mno haki ya kuwapo mgombea binafsi. Ilivyo ni kama haki hiyo haipo kwani imewekewa vizingiti vizito mno. Soma maneno haya ya Mwalimu Nyerere.

Ni ufisadi wa kutisha Geita

Viongozi wa kijiji wajichotea fedha ‘kiulaini’

 

Vigogo watatu wa Kijiji cha Mawemeru kilichopo katika Kata ya Nyarugusu, Wilaya ya Geita, mkoani hapa wanatuhumiwa kujigeuza “Miungu-watu” kwa kutafuna fedha za wanakijiji Sh 50 milioni.

Kwa nafasi hiyo, vigogo hao wanadaiwa kukigeuza kijiji hicho “shamba la bibi” huku wananchi wanaojitokeza kuhoji taarifa ya mapato na matumizi wakitishwa na wengine wakiishia kuswekwa ndani.

Vigogo waliokumbwa na tuhuma hizo ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji, Agness Matibu, Mwenyekiti wa Kijiji, Mussa Maduhu, pamoja na Mchumi, Philipo Kamuye, ambao, kwa kushirikiana wanadaiwa kutafuna kiasi hicho cha fedha.

Fedha hizo, zaidi ya Sh 50 milioni zinatokana na vyanzo vya ndani vya mapato yatokanayo na kijiji. Kadhalika sehemu ya fedha hizo hutokana na mapato yatokanayo na wawekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi.

Vyanzo vya gazeti hili vilidai kuwa vigogo hao kwa pamoja wameshirikiana kufisadi mapato ya kijiji na kwamba suala lolote linalohusu fedha zitokanazo na vyanzo hivyo, hakuna mwananchi anayeruhusiwa kuhoji na hawajawahi kusomewa taarifa za mapato na matumizi tangu mwaka 2011.