Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Dar es Salaam

Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) umesema Maonesho ya 48 ya Biasahara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yanafanyika katika Viwanja vya Julius Nyerere yamekuwa ya manufa ambapo hadi leo wamepima zaidi ya watu 300.

Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda wakati akizungumza na waandishi wa habari leo, ambapo amesema wananchi wameonesha uhitaji wa kujua majukumu ya wakala huo muhimu kwa maendeleo ya nchi.

Mwenda amesema katika maonesho hayo wamekuwa wakitoa huduma ya usajili, kupima afya na kuonesha vifaa ambavyo wanatumia vyenye ubora wa kimataifa.

“OSHA tumeshiriki kwenye maonesho haya ya 48, yamekuwa na mafanikio makubwa sana ndani hizi siku saba hadi nane za mwanzo, ambapo tunaendelea kusajili waajiri, kupima afya kwa zaidi ya watu 300 na kuonesha vifaa vyenye ubora, hali ambayo inavutia wawekezaji,” amesema.

Aidha, Mwenda amesema OSHA ipo katika hatua za mwisho za kuhakikisha mifumo yake inasomana na hWakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Deogratius Ndejembi ambalo alitoa alipotembelea banda la wakala huo.

Pia amesema OSHA inatumia mbinu ya majadiliano na waajiri katika utendaji huo, hali ambayo imewezeha kusajili sehemu nyingi za kazi.

Mtendaji mkuu huyo amesema hadi sasa wameweza kusajili sehemu za kazi 45,000, huku takribani sehemu za kazi 40,000 zikisajiliwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande mwingine Mwenda amesema katika mwaka huu wa 2024/25 OSHA itaongeza kasi ya kusajili na kukagua sehemu za kazi ikiwemo kwenye vyombo vya habari ambavyo ni wadau wa kubwa kwenye jamii.

Awali akizngumza na waandishi wa habari Waziri Ndejembi aliitaka OSHA na BRELA kuhakisha mifumo yao inasomana, ili kuleta tija zaidi katika utekelezaji wa majukumu.

Waziri Ndejembi amesema OSHA na BRELA zote ni taasisi za Serikali, hivyo katika keleta tija zinapaswa kusomana kwenye mifumo hali ambayo itapunguza mlolongo mrefu kwa wawekezaji.

“Napenda kutumia nafasi hii, kuwaelekeza OSHA kuwa mifumo yao inapaswa kusomana na BRELA, ili kurahisisha wawekezaji lakini pia kuokoa muda,” amesema.

Amesema hakuna haja ya OSHA kufika katika eneo la uwekezaji dakika za mwisho, bali inatakiwa kujua mapemba ili kuleta ufanisi katika kazi.

Ndejembi amesema iwapo taasisi hizi zitafanya kazi kwa pamoja ni wazi mafanikio ambayo Serikali inahitaji hasa katika huduma kwa wawekezaji yatafanikiwa.

Aidha, Waziri Ndejembi amewataka waajiri kujisajili OSHA, ili kuhakikisha wakala huyo anafanya ukaguzi ambao unahitajika kwenye sehemu za kazi na biashara kama sheria inavyotaka.

“Kusema kweli utendaji wa OSHA chini ya Mkurugenzi Khadija Mwenda na wasaidizi wake unaridhisha ndio maana unaona kasi ya usajili imeongezeka, endeleeni kukaza buti,” amesema.

Pia Waziri Ndejembi ameipongeza OSHA kwa kuzingatia weledi mkubwa katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku, huku akiitaka isifanye uaskari na kuwa marafiki wa waajiri, hasa kwa kuwekeza kwenye elimu hasa faida ya waajiri kujisajili kwao.

Amesema OSHA imekuwa na mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za kijamii na kuchochea ukaaji wa uchumi na kuitaka iongeze nguvu zaidi.

Please follow and like us:
Pin Share