Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Dar es Salaam

Katika kuunga mkonono juhudi za Rais Samia Suluhu Hasan, za kuchochea maendeleo, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), limedhamiria kuanzisha mkoa mpya wa kiutendaji wa Urafiki.

Akitangaza dhamira hiyo imeelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Hamad Abdallah, wakati akitoa taarifa kwa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo inayofanya ziara katika miradi mbalimbali kufahamu hatua za utekelezaji na changamoto.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa, mkoa huo mpya wa kiutendaji umelenga kuongeza uratibu bora wa shughuli za maendeleo na huduma kwa jamii katika eneo la Urafiki.

“Kuanzishwa kwa mkoa huo mpya utasaidia kuchochea maendeleo na kuboreshwa kwa huduma kwa jamii hayo yote ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia” amesema.

Pia amesema kuwa uanzishwaji wa mkoa huo utawezesha utoaji wa huduma bora za makazi na miundombinu muhimu kwa wakazi wa eneo hilo, pia kukuza fursa za kiuchumi na kijamii.

Amenongeza kuwa Urafiki ni moja kati ya maeneo yenye ukuaji wa haraka Jijini Dar es Salaam, na kuanzishwa kwa mkoa mpya wa kiutendaji kunatarajiwa kuongeza usimamizi thabiti na ufanisi katika utoaji wa huduma za maendeleo ya jamii na miundombinu ya makazi.

Mpango huu unakusudia pia kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wakazi wa Urafiki kwa kuimarisha mifumo ya utawala na usimamizi.

“Hatua hii inaonyesha dhamira ya NHC katika kuhakikisha maendeleo endelevu na ustawi wa jamii katika eneo la Urafiki, na inatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wenyeji wa eneo hilo na jamii kwa ujumla” amesema.

Akitoa taarifa fupi ya eneo la Urafiki, Mkurugenzi wa Usimamizi Miliki, Elias Msese amesema eneo hilo lina jumla ya Units 399 majengo ya biashara 6, makazi ya wataalamu 32, shule ya msingi, retail shop 32, maghala 31, yard za magari 10, gereji 4, kituo cha mafuta kimoja, sehemu za kuosha magari tatu. Industrial park. Kuna viframe vidogo vidogo na makontena.

Amesema kwa kuanzia shirika linaweza kukusanya kiasi cha shilingi bilioni moja kwa mwezi na kiasi hicho kitaongezeka kadri maboresho yanavyofanyika.

Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Sophia Kongela amepongeza hatua zote muhimu zilizopigwa baada ya makabidhiano na kutaka Shirika kufanya hatua za haraka zaidi ili kuliboresha eneo hilo.