WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, amesema taarifa ya miradi iliyobainika kuwa na dosari katika mbio za Mwenge wa Uhuru 2024, itakabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua zaidi.

Pia amesema katika maadhimisho ya wiki ya vijana kwa mwaka huu kutakuwa na makongamano kwa ajili ya vijana yanayolenga masuala mbalimbali ikiwamo elimu ya sera mpya ya maendeleo ya vijana toleo la 2024 na mafanikio ya miaka 60 ya Mwenge wa Uhuru.

Akizungumza jana na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho hayo, kilele cha mbio hizo sambamba na kumbukumbu ya miaka 25 ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere yatakayofanyika jijini Mwanza, Waziri Kikwete alisema kupitia mbio hizo, kumebainika kuwapo na dosari katika baadhi ya miradi ikiwamo kujengwa chini ya kiwango na kutokuwa na usimamizi mzuri.

“Taarifa ya miradi iliyotembelewa na Mwenge nitakabidhiwa kwa Rais Samia, siku ya kilele kwa hatua zaidi,” alisema.

Please follow and like us:
Pin Share