Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Dar es Salaam


Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imevunja rekodi kwa kutoa jumla ya Shilingi za Kitanzania 153.9 Bln kama gawio kwa Serikali kuu kwa mwaka wa fedha Mwaka 2023/2024.

Gawio hilo limeifanya TPA, kuongoza kwa kutoa gawio kubwa zaidi kuliko taasisi zote za Serikali hapa nchini, “na haya ni matunda ya uwekezaji uliofanywa katika Bandari ya Dar es Salaam”, amasema Mkurugenzi Mkuu, Bw. Prasduce Mbossa.

TPA imefanya uwekezaji mkubwa kwa kuboresha miundombinu ya kwa Bandari zake. Katika Bandari ya Dar es Salaam, TPA imefanya maboresho ya ujenzi wa magati na kuongeza kina, imetanua lango la kuingilia Bandarini na sehemu ya kugeuzia meli.

Mamlaka pia imekuwa ikishirikiana na vyema kiutendaji na wawekezaji ambapo hadi sasa Kampuni ya DP World imeshafanya uwekeza mkubwa kwa kununua vifaa kama SSGR (Ship to Shore Gang Cranes) nane (8), pamoja na T.T. (Terminal Tractors) 50.


Ushirikiano huo umefanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa, kuongeza ufanisi na kutoa huduma zake za kuhudumia meli na mizigo kwa ubora na ufanisi zaidi.

Please follow and like us:
Pin Share