Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema kuwa makubaliano yoyote ya amani kuhusu vita nchini Ukraine lazima yawe na dhamana ya usalama. Kauli hiyo alitoa alipokutana na Rais wa Marekani, Donald Trump, katika Ikulu ya White House kwa mazungumzo kuhusu mgogoro unaoendelea nchini Ukraine.
“Amani hii lazima isiwe kujisalimisha kwa Ukraine. Haitakiwi kuwa ni kusitishwa kwa mapigano bila hakikisho la usalama,” alisema Macron wakati wa mkutano wao wa pamoja wa waandishi wa habari baada ya mkutano wa Jumatatu.
Trump, ambaye hakutoa maoni kuhusu hakikisho la usalama moja kwa moja, alisisitiza kuwa gharama za kupata amani nchini Ukraine lazima zilitolewe na mataifa ya Ulaya na sio Marekani pekee.
Macron alijibu kwa kusema kuwa Ulaya inatambua umuhimu wa “kushiriki kwa usawa mzigo wa usalama,” akiongeza kuwa mazungumzo yanayoendelea kuhusu uvamizi wa Urusi yameonyesha njia ya kuendelea mbele na suluhisho la kisiasa.
Katika mkutano huo, baadhi ya tofauti za wazi ziliibuka kati ya viongozi wawili kuhusu namna ya kumaliza vita vya Ukraine. Wakati walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi ya Rais wa Marekani, Oval, walionyesha msimamo tofauti kuhusu njia bora ya kufikia amani.
