Isri Mohamed

Siku chache baada ya kutemwa na wekundu wa Msimbazi, aliyekuwa Winga wa Simba, Luis Miquissone amerejea kwenye klabu yake ya zamani ya UD do Songo kwa ajili ya msimu ujao wa 2024/25.

Miquissone amerejea UD do Songo baada ya kuwa nje kwa miaka minne akiiwakilisha Simba ya Tanzania (2020 na 2023), El Ahly ya Misri (2021 na 2023) na Abha Club kutoka Saudi Arabia (2022).

Kabla ya kuondoka Miquissone, Klabu ya Ud Songo ilishinda Kombe la Msumbiji mnamo 2016 na ubingwa wa kitaifa mnamo 2017.

Please follow and like us:
Pin Share