Naibu Waziri Nishati, Judith Kapinga Septemba 17, 2024 ameshuhudia fainali ya mashindano ya Doto Cup 2024 ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa.

Mashindano hayo yameandaliwa na Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko.

Mshindi katika fainali hiyo ni timu ya mpira wa miguu ya Butinzya ambayo mgeni rasmi aliikabidhi zawadi ya shilingi milioni tano, seti 3 za jezi na mipira mitatu.

Please follow and like us:
Pin Share