JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

KATIBA MPYA ITAKIMUDU KIZAZI CHA ‘FACEBOOK?’

“Nasema Katiba ya kweli ya Watanzania inapaswa kuandikwa katika mioyo na utashi wao, na wala si ya kuandikwa kama hii tunayoililia sasa”.

Operesheni za al-Shabaab zadhoofishwa Kenya

Operesheni za usalama zinazofanywa kwa msaada na jamii zimedhoofisha uwezo wa kundi la wanamgambo la al-Shabaab kufanya mashumbulizi nchini Kenya. Tangu Februari 17, wakati wanachama wa al-Shabaab waliposhambulia kituo cha polisi katika eneo la Jarajila mjini Garissa, na kumuua polisi mmoja, hapajatokea mashambulizi yoyote yanayohusishwa moja kwa moja na al-Shabaab katika eneo hili, Kamishna wa Jimbo la Kaskazini Mashariki, James ole Seriani, alisema mwishoni mwa wiki.

Hongera MCT, lakini namna ya kuwapata washindi itazamwe

Baraza la Habari Tanzania (MCT) limetoa tuzo kwa waandishi wa habari, wachora katuni na wapigapicha bora. Hili ni tukio jema. Linapaswa kuungwa mkono. Rais Jakaya Kikwete ameliona hilo, ameahidi kuwa Serikali itashiriki.