JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Wamiliki wa daladala na machozi yasiyokauka

Baada ya kununua basi dogo (Hiace) la kwanza na kulisajili daladala, nilikutana na ulimwengu mpya wa changamoto za biashara za magari. Changamoto zilipozidi niliazimu kukutana na walionitangulia kwenye biashara hiyo ili nipate hazina ya ushauri.

Baraza la Kata Kwashemshi tupewe semina

Mimi ni msomaji wa Gazeti Jamhuri. Naishi hapa Kwashemshi wilayani Korogwe. Kinachosikitisha ni kwamba tangu mwaka jana tuteuliwe katika Baraza la Kata hakuna semina yoyote ambayo wajumbe tumepewa.   Sasa inatuwia vigumu kwetu kutafsiri sheria. Hali hii ni kinyume kabisa…

Bongo: Matendo kwanza

“Ni wajibu wa viongozi wa Afrika kuonyesha utashi wao wa kisiasa, kwa ajili ya kuhakikisha taasisi za umajumui wa Kiafrika (pan-African) unakuwa chombo murua na kisiwe chombo cha mijadala isiyo na ukomo.”

Haya ni maneno ya aliyekuwa Rais wa Gabon, Omar Bongo, aliyefariki mwaka 2009 baada ya kuitawala nchi hiyo kwa muda mrefu.

Taifa letu lipo njia panda

*Bunge, wabunge, vyombo vya habari, wananchi tujadili

Ninakumbuka baadhi ya michango ya mjadala juu ya bajeti ya mwaka 2012/2013 na jinsi ilivyokuwa ya kichama zaidi kuliko uhalisia. Wabunge wetu walisahau kabisa kusudi kubwa kati ya yaliyowaweka bungeni, yaani utashi wa nchi, kwa maana ya uwakilishi wa mamilioni ya Watanzania waliowaamini na badala yake kwa kiwango kikubwa wakatekeleza utashi wa sera za vyama vyao na utashi binafsi.

Njooni shambani mtajirike

Miezi kadhaa iliyopita kupitia Redio TBC Taifa, ofisa mmoja wa Wizara ya Maliasili na Utalii aliulizwa swali hili, “Je, inawezekana watu binafsi kufungua mashamba ya miti na kufanya biashara ya kuuza miti ya mbao?”

Siri zaanza kuvuja rushwa Kamati za Bunge

 

Mtandao wa wafanyabiashara wahusishwa

Kamati ya Maliasili, Mazingira yaguswa

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira aliyejitambulisha kuwa ni mpinga vitendo vya rushwa, ameamua kuandika makala hii kueleza baadhi ya vitendo vya rushwa ndani ya Kamati hiyo. Hii ni sehemu ya makala ya mbunge huyo ambaye kwa sasa tunalihifadhi jina lake.

UTANGULIZI

Tarehe 28 Julai 2012, Bunge la Tanzania liliingia katika historia baada ya Spika Anne Makinda kutangaza kuivunja Kamati ya Nishati na Madini pamoja na kamati nyingine zinazotuhumiwa kwa rushwa.

Spika alifikia hatua hiyo baada ya kuwapo kwa harakati za wafanyabiashara wa sekta ya mafuta kufanya mipango kwa zaidi ya wiki mbili za kuwashawishi wabunge washinikishe kujiuzulu kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, na Katibu Mkuu Eliakim Maswi kwa kile kinachodaiwa kutoa zabuni kwa kampuni ya Puma Energy ya kuiuzia mafuta Tanesco kwa ajili ya mitambo ya umeme wa dharura ya  IPTL. Harakati zililenga wabunge wengi wenye ushawishi bungeni, wakianzia na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya