JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Dk. Hoseah aomba majina ya walioficha mabilioni Uswisi

 

*Asema Takukuru haizuii watu kujenga mahekalu

*Wadau wataka wanaothibitika kula rushwa wauawe

 

Ujasiri na ushirikiano wa dhati vimetajwa kuwa ni miongoni mwa nyenzo thabiti, zinazoweza kuongeza ufanisi katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa nchini.

 

Afadhali ya ‘ngangari’ kuliko ‘magwanda’ haya (1)

Si siri kuwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini, mambo si shwari. Amani na utulivu wa nchi yetu vimetikisika. Nadiriki kusema hivi kwa sababu, tangu Uchaguzi Mkuu wa kwanza uliofanyika mwaka 1995, amani na utulivu vimekuwa vikiyumba kila kukicha.

Wingi wa sukari maghalani wamkera Waziri Chiza

 

*Ahoji sababu ya kutouzwa, akerwa na bei ghali ya sukari

*Akataa kuruhusu iuzwe nje, Mkurugenzi wa Bodi amkwaza


Wakati Watanzania wakiumizwa na bei ghali ya sukari, imebainika kuwa karibu tani 180,000 za bidhaa hiyo ‘zinaozea’ maghalani katika Jiji la Dar es Salaam na sasa wafanyabiashara wanasaka kibali cha kuiuza nje ya nchi.

Baada ya Ziwa Nyasa, mgogoro sasa waibuka Ziwa Kitangiri

Umiliki wa Ziwa Kitangiri unafanana na mgogoro uliopo sasa wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi katika Ziwa Nyasa. Wakati mgogoro wa Malawi ukipewa kipaumbele, huu wa Ziwa Kitangiri linalotenganisha wilaya za Meatu na Iramba haujapewa msukumo wa kutosha.

Wanasiasa wengi wanatafuta ulaji, si uongozi

 

Wakati zamani dhamira ya wanasiasa wengi ilijikita katika kutafuta uongozi wa kutumikia umma, siku hizi mambo ni tofauti. Wengi wao wanasaka uongozi kwa lengo la kujipatia ulaji! Nani anapinga? Fuatilia kwa makini viongozi wa kisiasa nchini hususan kuanzia ngazi ya kata, jimbo hadi Taifa utaona wengi wao wanatumia nyadhifa zao kujitafutia maslahi binafsi ya kujineemesha na familia zao.

Elimu ya Tanzania vipi? (3)

Kwa hizi kazi za taaluma (professionals) kama ualimu, udaktari, ufundi, sheria, kilimo na kadhalika zina kima chake cha kuhitimu.