JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Baada ya Ziwa Nyasa, mgogoro sasa waibuka Ziwa Kitangiri

Umiliki wa Ziwa Kitangiri unafanana na mgogoro uliopo sasa wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi katika Ziwa Nyasa. Wakati mgogoro wa Malawi ukipewa kipaumbele, huu wa Ziwa Kitangiri linalotenganisha wilaya za Meatu na Iramba haujapewa msukumo wa kutosha.

Wanasiasa wengi wanatafuta ulaji, si uongozi

 

Wakati zamani dhamira ya wanasiasa wengi ilijikita katika kutafuta uongozi wa kutumikia umma, siku hizi mambo ni tofauti. Wengi wao wanasaka uongozi kwa lengo la kujipatia ulaji! Nani anapinga? Fuatilia kwa makini viongozi wa kisiasa nchini hususan kuanzia ngazi ya kata, jimbo hadi Taifa utaona wengi wao wanatumia nyadhifa zao kujitafutia maslahi binafsi ya kujineemesha na familia zao.

Elimu ya Tanzania vipi? (3)

Kwa hizi kazi za taaluma (professionals) kama ualimu, udaktari, ufundi, sheria, kilimo na kadhalika zina kima chake cha kuhitimu.

Nyerere: Ubovu wa CCM

“Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa vyama vingi.  Nilitumaini kuwa tunaweza kupata chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha CCM kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao.”

Haya ni maneno ya Mwasisi na Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Nyerere, wakati akiwahusia viongozi wa CCM kujirekebisha na kutumikia wananchi.

Kampuni za kigeni zinavyosulubisha za wazawa

Wakati fulani kule nchini Marekani kulitokea malumbano makali baina ya kampuni za Brother na Smith Corona zenye nguvu na ushindani mkali. Kampuni hizo zinajishughulisha na utengenezaji wa bidhaa zinazofanana zikiwamo mashine za kuchapa (typewriters), vichapishi (keyboards) za kompyuta, viyoyozi na vifaa lukuki vya kielektroniki.

Papa John Paul II: Mapadre si wanasiasa

“Ninyi ni wachungaji, si viongozi wa kijamii wala viongozi wa kisiasa. Hebu tujiepushe na mihemko itakayotufanya kuchanganya huduma ya Mungu na masilahi ya kupita yaliyotiwa chumvi.” Haya ni maneno ya Baba Mtakatifu Papa John Paul II alipokuwa akiwaasa wachungaji na…