JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Wanafunzi masikini wanyimwa mikopo

Wakati vyuo vya elimu ya juu vimeanza mapokezi ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza wiki iliyopita, wanafunzi wengi hasa kutoka familia maskini bado wako nyumbani huku wakihofia kukosa masomo baada ya kukosa mikopo.

Tujihadhari unafiki usitunyime rais bora 2015

Uchaguzi Mkuu ujao hauko mbali kiasi cha kufanya Watanzania wachelewe kuanza maandalizi mapema. Ndiyo maana wengi hatushangai kuona na kusikia wanasiasa wanaojipanga sasa kwa ajili ya uchaguzi huo.

Utaifa hauna dini (2)

Licha ya kuwa na huo msimamo usiofungamana na dini yoyote, kati ya hizo mbili -uislamu wala ukristu- makundi yote mawili wakati ule waislamu wenye Koranic Schools ukanda wa mwambao hawakuzipokea shule hizi za Serikali.


Na wamisheni kwa wakati huo huo wakailaumu Serikali eti kwanini walianzisha shule hizi zenye mwegemeo wa kuwapendeza waislamu wale wa mwambao. Mawazo potofu kama haya yanaonekana katika maandishi mbalimbali ya wakati ule toka kila upande.

Uuzwaji ardhi Bagamoyo waitisha Serikali

 

* DC atoa tamko kali, awaonya wavamizi

* Ataka wanunuzi wafuate kanuni, sheria

* Ashauri wenyeji wabakize ya kuwasaidia

* Mifugo yailemea wilaya, aipiga marufuku


Serikali katika Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, imewataka wananchi wawe makini katika uuzaji ardhi, kutokana na wimbi la Watanzania na raia wa kigeni wanaojitwalia ardhi kubwa wilayani humo.

 

Nyerere: Vyombo vya umma

“Vyombo vya umma vitumiwe kuhudumia wananchi. Wote wanaoviharibu ama kwa bahati mbaya ama kwa makusudi, lazima wajisahihishe; la sivyo wanyang’anywe madaraka.”

Ni maneno ya mwasisi na Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Nyerere, alipowaasa viongozi kutumia vizuri madaraka yao kwa kuhakikisha vyombo vya umma vinahudumia wananchi kwa uzito unaostahili.

Waziri Mwakyembe alikosea kuhamishia ofisi kanisani

 

Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ni miongoni mawaziri wachache wanaoheshimika nchini, kutokana na jitihada kubwa anazofanya katika kuwatumikia wananchi.