JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Dalili ya kudidimia kwa uongozi bora Afrika

 

TUZO YA MO IBRAHIM KUKOSA MSHINDI

 

Nimesikitishwa na habari za Tuzo ya Mo Ibrahim kukosa mshindi mwaka huu, zilizotangazwa hivi karibuni na Kamati ya tuzo hiyo ambayo ni zawadi yenye thamani kubwa dunaini. Tuzo hiyo ilianzishwa mwaka 2006 na bilionea wa nchini Sudan, Mo Ibrahim, kwa ajili ya marais wastaafu wa nchi za barani Afrika.

 

JKT ni mtima wa Taifa (1)

Nimefurahishwa sana na tamko la Mkuu mpya wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael Muhuga, alilolitoa Ikulu Septemba 26, mwaka huu, mara tu baada ya kuapishwa kwake kushika wadhifa huo.

Ushindi mgogoro Ziwa Nyasa ni wetu – Membe

*Wazee wataka waruhusiwe watumie ‘nguvu za miujiza’

“Inawezekana shetani kaingia. Huku Tanzania tuna uwezo hata wa kutumia ungo…mimi nimekulia hapa, mpaka ni katikati ya ziwa…Kama ninyi (Serikali) hamna bunduki, wananchi wapo tayari kupigana kwa kutumia fito…Hatutakufa mpaka tuone mwisho wa mgogoro huu, tupo tayari hata kwa kutumia miujiuza yetu,” Haya ni maneno ya  Mzee Anyosisye Mwakenja (80) wa Kijiji cha Matema Beach.

Watanzania tunapaswa kuongeza ‘akili ya fedha’

Mapema Julai mwaka huu, nilikutana na mzee mstaafu kutoka moja ya wilaya za mkoani Iringa. Mzee huyu ambaye ndiyo kwanza amestaafu  ualimu, nilimfahamu kwa njia ya simu kupitia kwa rafiki yangu. Haja ya mzee huyu ilikuwa tukutane nimsaidie kutafuta gari aina ya Hiace anunue.

Trafiki wanakula kwenye daladala Dar es Salaam?

*Baadhi ya madereva, makondakta ni miungu watu

Usafiri wa daladala katika Jiji la Dar es Salaam siku hizi ni mithili ya mfupa unaoelekea kumshinda fisi. Baadhi ya madereva na makondakta ni miungu watu! Sijui wanakula pamoja na askari wa usalama barabarani (trafiki)?

Utaifa hauna dini (4)

Nadhani kila anayesoma maneno haya hii leo, anaweza kuona jinsi Baba wa Taifa alivyodhamiria kujenga nchi ya watu wenye hali ya usawa katika kila nyanja.