Category: Makala
Maazimio Mkutano Mkuu: Kitanzi kinachoisubiri CCM
*Imeagiza bei za vifaa vya ujenzi zishushwe nchini
*Tofauti ya kipato yaelezwa ikiachwa hivi italeta vurugu
*Ada shule binafsi zidhibitiwe, utozaji dola ukomeshwe
*Yakiri ajira ni bomu, wizara lazima ziandae ajira mpya
*Ushuru na vijikodi vinavyoumiza wananchi vikomeshwe
Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mkutano wake Mkuu wa Nane uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma, kilitoa maazimio ambayo kimeyaeleza kuwa ndiyo dira yake ya ushindi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Wadau waaswa kuhusu takwimu sahihi
Sekta za umma, binafsi na wadau wa maendeleo kwa jumla, wameshauriwa kuzingatia matumizi bora kuwezesha upatikanaji wa takwimu sahihi na fursa kwa jinsia zote katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Nyangwine: Sijaitelekeza Tarime
*Ajivunia maendeleo aliyowezesha
Mbunge wa Tarime mkoani Mara, Nyambari Nyangwine (CCM), ameibuka na kukanusha tuhuma za kutelekeza jimbo hilo kwa zaidi ya miezi sita mfululizo.
Mapya yaibuka Tundu Lissu vs majaji vihiyo
*Yumo aliyeghushi umri, atang’atuka mwaka 2017
*Mwingine ahitimu chuo kikuu na kupewa ujaji
Miezi kadhaa baada ya JAMHURI kuchapisha taarifa ya utetezi wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), kuhusu uteuzi wa majaji wasio na sifa, mbunge huyo ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Upinzani na Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa Wizara ya Katiba na Sheria, wiki iliyopita alijitokeza tena na kutishia kumshitaki Rais Jakaya Kikwete.
JKT ni mtima wa Taifa (2)
Vijana waliongia baada ya wale wa kwanza walipewa majina mbalimbali, maana kazi yao kubwa ilikuwa kujenga Taifa na si kuziba nafasi katika Jeshi la Ulinzi. Novemba 1964 waliingia vijana zaidi ya 400 na hawa waliitwa “Mkupuo Maendeleo” (Operation Maendeleo). Ndiyo hasa waliofungua kambi mbalimbali za uzalishaji mali katika JKT.
Raha ya garimoshi la Mwakyembe
Kama ilivyo kwa nchi nyingine nyingi duniani, sekta ya usafiri wa reli ni muhimu katika kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi.