JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Mwalimu Nyerere: Kujitolea kumefifia

“Siku hizi kuna watu wengi mno ambao huingia katika chama na kugombea nafasi za uongozi kwa matumaini ya kupata fedha na vyeo kwa faida zao wenyewe. Moyo wa kujitolea umefifia mno. Katika hali kama hiyo ni vigumu sana kuwapata viongozi wenye moyo wa kuwatumikia wenzao.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Nyerere, wakati akikemea tabia ya wanaotafuta uongozi kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Alizaliwa Aprili 13, 1922 kijijini Butiama, Mara, alifariki Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza.

Julius Nyerere: Tukiendeleze Kiswahili

“Pamoja na kwamba mimi binafsi napenda tuendelee kufundisha Kiingereza katika shule zetu, kwa sababu Kiingereza ndicho Kiswahili cha Dunia, tuna wajibu mkubwa kuzidi kukiendeleza na kukiimarisha Kiswahili: Ni silaha kubwa ya umoja wa Taifa letu.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, yanayopatikana katika moja ya hotuba zake kwa umma. Alizaliwa Aprili 13, 1922 kijijini Butiama, Mara na kufariki Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza.

Kuna umuhimu wa wafanyabiashara ‘kuolewa Bongo’

Novemba 11, mwaka huu, nilikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria semina ya biashara na ujasiriamali katika ukumbi wa Matumaini Centre, uliopo Sabasaba Iringa mjini. Semina hii iliendeshwa na mtaalamu na mshauri wa kimataifa wa masuala ya biashara na ujasiriamali, Perecy Ugula, kupitia kampuni yake ya Great Opportunity Consulting Limited (GOC Ltd).

Serikali isipuuze, udini upo, iudhibiti

Naanza maelezo yangu kwa kusema yafuatayo: Msema kweli hukimbiwa na marafiki zake; siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo; nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.

Kinana umeanza vizuri, uendelee, umalize vizuri

Nilikuwa naelekea kukata tamaa kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakitakuwa na viongozi wanaokerwa na umaskini unaoendelea kuwanyima Watanzania wengi maendeleo ya kweli.

JKT ni mtima wa Taifa (3)

Nimejaribu kurejea kirefu maneno ya Mwalimu kuonesha uchungu wake kwa wasomi waliosema miili itakwenda, lakini mioyo yao haitakuwa huko National Service.