JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

JKT ni mtima wa Taifa (5)

 

JKT ni mtima wa Taifa (5)Napenda kukumbusha wahusika kuwa wakati utaratibu wa kuwaita vijana kwa mujibu wa sheria ukiandaliwa katika ile (White Paper No. 2 ya mwaka 1966), katika ibara ya 9, kulianishwa masomo ya kuwafundisha vijana wote katika JKT.

Tamaa ya utajiri yachochea ushirikina migodini Geita

“Ushirikina huku Geita ni mkubwa, wachimba madini wengi wanaamini hawawezi kufanikiwa bila kufanya ushirikina, ndio maana kuna vitendo vya mauaji ya alibino na kukata viungo vyao.”

Hiyo ni kauli ya mchimbaji mdogo wa dhahabu katika mgodi wa Nyarugusu alipozungumza na JAMHURI hivi karibuni, kuhusu ukubwa wa imani za ushirikina kwa wachimbaji wadogo wa madini mkoani Geita.

Kwa hili nasimama na David Cameron

NAANDIKA makala hii nikiwa jijini Manchester kwa shughuli maalumu ya kimichezo, nikiwa mdau kiasi. Naandika nikiwa bado na tafakari nzito na hofu juu ya hali ya vyombo vya habari vya Uingereza huko tuendako.


Fursa ya biashara ya mtandao duniani

Nianze kwa kuwasalimu wasomaji wetu ambao mmekuwa mkifuatilia safu hii kwa umakini mkubwa. Niwashukuru kipekee wote wanaonipigia simu, kuniandikia ujumbe mfupi (SMS) na baruapepe. Michango yenu wasomaji ina msaada mkubwa sana katika maeneo matatu.

Mosi, inanipa taarifa kwamba ninachokiandika kinasomwa.

Serikali isipuuze, udini upo, iudhibiti – 2

Inatoka toleo lililopita.

Jicho la kulia linaona dini ni mojawapo ya ngao zake katika kuwadhibiti na kuwahukumu raia wake wenye kutenda maovu au kwenda kinyume cha sheria za dola.

Baadhi ya maazimio ya CCM yametuhadaa

Ni jambo zuri kuona na kusikia Mkutano Mkuu wa Nane wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umetoa maazimio ya kukiimarisha chama hicho tawala na kushughulikia changamoto mbalimbali nchini.