Category: Makala
Sagara: Katiba izuie wastaafu kurejeshwa kazini
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Amos Sagara (pichani chini), amependekeza Katiba mpya izuie wastaafu kurejeshwa katika utumishi wa umma.
Utawala Bora hutokana na maadili mema (2)
Mara baada ya Uhuru baadhi ya wageni kwa dharau za makusudi kabisa walijaribu kuchezea uwezo wa Serikali ya Taifa letu huru. Nitoe mifano ya dharau za namna hiyo.
NUKUU ZA WIKI
Nyerere: Viongozi wabovu hulizwa na matatizo
“Viongozi wabovu wenye mioyo ya kuku, hulizwa na matatizo; bali watu madhubuti, wenye mioyo thabiti, hukomazwa nayo… hatima ya nchi yetu ni jukumu letu. Kwa pamoja tunaweza kuisaidia nchi yetu kusonga mbele kuelekea kwenye haki zaidi na usawa zaidi kwa Watanzania wote.”
Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Biashara zinahitaji utaalamu, sio kupapasa
Kwa muda mrefu sasa, nimejijengea utamaduni wa kujisomea vitabu. Sisomi kila aina ya vitabu, isipokuwa ninapenda sana vitabu vya biashara na uchumi (finance, economic, entrepreneurship and business), vya uhamasisho na shuhuda (motivational and inspirational) na vinavyohusu ustawi wa kiroho na kimaisha (spiritual and personal improvements). Mara chache sana huwa nasoma vitabu vinavyohusu siasa hasa zile za kimataifa.
Mtendaji Mkuu OSHA matatani
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Dk. Akwilina Kayumba, anahusishwa na matumizi mabaya ya madaraka na ya fedha za umma.
Ni ujinga CHADEMA kupinga uzazi wa mpango
Desemba 31, 2012 Rais Jakaya Kikwete alitangaza matokeo ya sensa ya watu na makazi, iliyofanyika Agosti mwaka huo. Rais Kikwete alitangaza kwamba kwa mujibu wa matokeo ya sensa hiyo idadi ya Watanzania ni 44,929,002.