JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Obama ampandisha chati Lowassa

Hatua ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion Ubungo jijini Dar es Salaam, imeamsha mjadala mzito katika jamii uliowafanya Watanzania kuanza kumhurumia Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wakiona alionewa.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Mahitaji ya wananchi yalindwe

“Lazima tuendelee kuhakikisha kwamba mahitaji ya msingi ya watu wote yanapatikana na yanalindwa. Lengo letu lazima liendelee kuwa kuinua hali ya maisha ya kila mtu, na kila mtu aweze kupata huduma za msingi za elimu na matibabu.”

Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Hoja ni kutii sheria, si kufuta kauli

Hivi karibuni niliandika makala nikizungumzia kauli za wanasiasa na athari zake kwa umma. Nilizungumza kuhusu kauli zinazochochea vurugu, migongano na kuleta chuki na uvunjifu wa amani.

Mandela alifunguliwa milango ya gereza, akagoma kutoka

Ikiwa Mungu atapenda, maana hadi tunachapisha makala haya, Mzee wetu, mwana wa kweli wa Afrika, Nelson Rolihlahla Mandela maarufu kama Madiba, wa Afrika ya Kusini, Alhamisi wiki hii atatimizi miaka 95 ya kuzaliwa. Mandela anaumwa akisumbuliwa na ugonjwa wa maambukizi ya mapafu na amelazwa katika hospitali moja jijini Pretoria, nchini humo.

Utajiri wa Loliondo na laana yake (2)

 

Mfululizo huu wa makala kuhusu Loliondo ulianza wiki mbili zilizopita. Kwenye toleo la mwisho, tuliishia kwenye kipengele kinachopingana na propaganda za uongo kwamba Serikali imechukua ardhi ya vijiji. Mwandishi anasema baadhi ya madiwani na NGOs zimetumiwa kueneza uongo huo kwa maslahi yao ya kisiasa na kiuchumi. Endelea.

Mwalimu Nyerere alijua ujio wa Obama tangu mwaka 1967

Mwaka huu pekee, Tanzania imepokea marais wa mataifa mawili makubwa yanayoongoza kwa uchumi imara duniani. Rais Xi Jinping wa China alikuwa wa kwanza, na baadaye amefuatiwa na Rais Barack Obama wa Marekani. Ujio wa viongozi hao, pamoja na kauli za kwamba wanataka kufungua milango ya kushirikiana kiuchumi, ni ukweli ulio wazi kwamba Tanzania imeendelea kurusha ndoana ya kuomba misaada. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, katika hotuba yake ya Februari 5, 1967 jijini Dar es Salaam, alieleza athari za nchi kuwa omba-omba. Sehemu hii ya hotuba inapatikana kwenye kitabu chake cha Ujamaa ni Imani (2). Endelea.