Category: Makala
JE, KESHO YA MJASIRIAMALI INATABIRIKA?
Mara nyingi ninapochambua masuala haya ya Biashara na Uchumi huwa ninakwama kupata maneno yaliyozoeleka katika Kiswahili ili kuelezea dhana fulani fulani. Hii haimaanishi kuwa Kiswahili hakina maneno hayo, la hasha! Isipokuwa kutumia maneno hayo kunaweza kuwapoteza wengi na kutoeleweka kirahisi.
Tanzania iwe kwa Watanzania kwanza
Chama cha Tanganyika African National Union (TANU) kilichodai Uhuru wa nchi hii kilikuwa na ahadi nzuri. Baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilizirithi.
Matatizo ya sekta ya vitabu Tanzania
Kama tujuavyo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeanza kutekeleza mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), huku Taifa likiwa na matatizo makubwa ya kuwapo kwa vitabu vibovu shuleni. Ni matatizo yaliyotokana na sera mbovu ya vitabu Tanzania.
Kumbe ndio maana trafiki wanachukiwa
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikisikia na kuona jinsi wananchi wengi katika maeneo mbalimbali ya nchi hii, wanavyowalalamikia askari polisi wa kitengo cha usalama barabarani (trafiki). Siyo siri ndugu zetu hao wanachukiwa na wananchi wengi.
Vidonda vya tumbo na hatari zake (13)
Katika toleo la 12 la mfululizo wa makala haya, Dk. Khamis Zephania alieleza dalili za tumbo kujaa gesi na tatizo la kufunga choo. Sasa endelea kumfuatilia katika sehemu hii ya 13.
Kesi kubwa ya ‘unga’ yatajwa Dar
*Ni ya Mama Lela aliyetajwa na Rais Obama
Kesi ya mtuhumiwa mkubwa wa dawa za kulevya duniani aliyekamatwa eneo la Mbezi jijini Dar es Salaam imetajwa wiki hii.
JAMHURI ilipata taarifa kutoka Mahakama Kuu kuwa kesi hii, inahusisha watuhumiwa wanane akiwamo Mtanzania Mwanaidi R. Mfundo. Pia nchini Kenya na Marekani anafahamika kwa jina la Naima Mohamed Nyakiniywa au Naima Nyakinywa, maarufu Mama Lela huko Mbezi, jijini Dar es Salaam akiwa pamoja na Wakenya saba, imetajwa jana Mahakama Kuu.