Category: Makala
Fedha zako ni kipimo cha imani yako
Nianze kwa kuwasalimu wasomaji wetu. Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mchakato wa Katiba mpya, lakini ninasikitishwa na namna mwenendo wa Bunge hilo ulivyo.
Wiki iliyopita tumeshuhudia mgogoro wa kimakundi uliosababisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kususia vikao vya Bunge Maalum la Katiba.
Binafsi ninaamini kuwa pande zote zitakaa chini na kufikia mwafaka ili Taifa letu lipate Katiba mpya.
Sasa tuendelee na uchambuzi wa leo unaohusu uhusiano wa imani zetu na umilikaji fedha.
Tangu lini wapinzani wanawapenda wananchi?
Vyama vya upinzani vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) katika Bunge Maalum la Katiba vimesusia vikao vya bunge hilo tangu Aprili 16, mwaka huu.
Wapinzani wametoa sababu zao za kuchukua hatua hiyo. Kwa mfano, wamesema Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, wametoa vitisho kwamba kukiwapo Serikali tatu Jeshi litachukua nchi.
Nani analinda bodaboda Dar?
Moja ya mambo yaliyomfurahisha Mkata Mitaa (MM) ni hatua iliyochukuliwa na Serikali kupiga marufuku pikipiki maarufu kwa jina la ‘bodaboda’, mikokoteni (makuta), baiskeli na bajaj kuingia katikati ya jiji la Dar es Salaam.
MM amefurahishwa na mpango huo kutokana na boda boda kuwa kero kwa waendesha magari na waenda kwa mguu wanaotumia barabara za katikati ya jiji.
Vituko vya DC Geita vyaongezeka – 3
DC adaiwa kumtisha Roboyanke
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyara, Makoye Roboyanke (CCM), ambaye inadaiwa alivuliwa madaraka hayo na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie, amedai kuwa Septemba 10, 2013 mchana akiwa shambani kwake kijijini hapo, alipokea simu ya vitisho kutoka kwa kiongozi huyo wa Serikali.
“Alijitambulisha kwa jina moja la Mangochie na kwamba ndiye Mkuu wa Wilaya ya Geita, akaniuliza jina langu nami nikamjibu… akaniuliza ninachofanya kwa wakati huo na kazi yangu hasa ni nini, nikamwomba arekebishe kauli, na baada ya kurekebisha kauli na kuniuliza maswali ya msingi nilimpa ushirikiano.
KAGAME NI MTIHANI
Viongozi Maziwa Makuu waufanye kwa Uangalifu – 4
Tangu Kagame na RPF waitwae Rwanda ni wazi kuwa nchi hiyo inapokea fadhila za Washington DC kuliko nchi yoyote nyingine katika Maziwa Makuu.
Misaada ambayo inatoka Marekani na Uingereza kuelekezwa Kigali ni mingi na ya aina mbalimbali. Kwa hesabu rahisi misaada hiyo inafafanua ustawi wa uchumi wa Rwanda tunaouona leo.
JWTZ: Tunavifyeka vikundi vya waasi Congo
Baada ya ushindi dhidi ya Waasi wa March 23 (M23), Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na Majeshi ya Umoja wa Mataifa (MUNUSCO) limesema hakuna kikwazo chochote cha kuwaondoa waasi wa ADF- NALU na FDRL.