Category: Siasa
Nyerere: Vipimo vya utajiri
“Kupima utajiri wa taifa kwa kutumia vigezo vya pato la taifa ni kupima vitu, si ufanisi.”
Haya ni maneno ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoyatoa Januari 2, 1973 jijini Khartoum, Sudan katika mkutano wa kuimarisha pato la taifa kwa nchi za ukanda wa kusini mwa Jangwa la Sahara.
Afadahi ya ‘ngangai’ kuliko ‘magwanda’ haya (2)
Lema akashinda. Lakini kutokana mwenendo wa kampeni ulivyokuwa, makada wa CCM ambao hawakuridhika, wakafungua kesi Mahakama Kuu na Lema akapigwa chini. Kama kawaida, wafuasi wa Chadema wakiwamo wana harakati na baadhi ya wasomi, wakamsuta Jaji aliyetoa hukumu hiyo kwa madai kuwa ilifanyika kisiasa.
Wanafunzi masikini wanyimwa mikopo
Wakati vyuo vya elimu ya juu vimeanza mapokezi ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza wiki iliyopita, wanafunzi wengi hasa kutoka familia maskini bado wako nyumbani huku wakihofia kukosa masomo baada ya kukosa mikopo.
Tujihadhari unafiki usitunyime rais bora 2015
Uchaguzi Mkuu ujao hauko mbali kiasi cha kufanya Watanzania wachelewe kuanza maandalizi mapema. Ndiyo maana wengi hatushangai kuona na kusikia wanasiasa wanaojipanga sasa kwa ajili ya uchaguzi huo.
Utaifa hauna dini (2)
Licha ya kuwa na huo msimamo usiofungamana na dini yoyote, kati ya hizo mbili -uislamu wala ukristu- makundi yote mawili wakati ule waislamu wenye Koranic Schools ukanda wa mwambao hawakuzipokea shule hizi za Serikali.
Na wamisheni kwa wakati huo huo wakailaumu Serikali eti kwanini walianzisha shule hizi zenye mwegemeo wa kuwapendeza waislamu wale wa mwambao. Mawazo potofu kama haya yanaonekana katika maandishi mbalimbali ya wakati ule toka kila upande.
Uuzwaji ardhi Bagamoyo waitisha Serikali
* DC atoa tamko kali, awaonya wavamizi
* Ataka wanunuzi wafuate kanuni, sheria
* Ashauri wenyeji wabakize ya kuwasaidia
* Mifugo yailemea wilaya, aipiga marufuku
Serikali katika Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, imewataka wananchi wawe makini katika uuzaji ardhi, kutokana na wimbi la Watanzania na raia wa kigeni wanaojitwalia ardhi kubwa wilayani humo.