Category: Siasa
Biashara inahitaji ramani sahihi
Wiki iliyopita wakati nikiangalia taarifa ya habari katika moja ya vituo vya televisheni hapa Tanzania, nilikutana na habari kuhusu wakulima wa mpunga walioandamana hadi Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.
KAULI ZA WASOMAJI
Stendi ya Nyegezi ni jehanamu
Stendi ya mabasi ya Nyegezi, Mwanza ni mithili ya jehanamu, utapeli na usumbufu vimekithiri. Kwanini stendi za Tanzania zimeachwa kuwa vituo vya uhalifu wa kila aina, huku polisi wapo? Uchunguzi zaidi ufanyike kusaidia wananchi.
Rwambali F, Mwanza
NUKUU ZA WIKI
Nyerere: Jeshi letu ni la Kizalendo
“Jeshi letu haliwezi kuwa Jeshi la mamluki, ni Jeshi la Kizalendo. Matumaini yangu ni kwamba Jeshi letu litaendelea kulinda na kutetea misingi mikuu ya Azimio la Arusha.”
Maneno haya ni ya Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye pia ni mwasisi wa Azimio la Arusha.
Wabunge wa CCM wameshindwa kazi?
Sina sababu yoyote ya kuwavunjia heshima wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Lakini katika enzi hizi za ukweli na uwazi sioni, sababu ya kusita kuzungumzia masuala nyeti kwa ukweli na uwazi. Lengo langu ni kuwaomba waone ugumu wa uchaguzi wa mwaka 2015.
Bila uwajibikaji Tanzania tutakwama (1)
Baada ya kusoma mengi katika magazeti na kuona kwenye runinga namna lile jengo la ghorofa 16 lilivyoporomoka, mimi, huenda na wengine wengi. tumeingiwa na wasiwasi.
AMREF yajizatiti kuboresha afya ya mama na mtoto Simiyu
Dalili za kufikia mafanikio ya kuboresha afya ya kina mama na watoto katika Mkoa mpya wa Simiyu, zimezidi kuonekana baada ya Shirika la Tafiti na Dawa Afrika (AMREF) kuwakutanisha wadau huduma za afya.