JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Kujitolea muhimu kwenye chama

“Lakini chama chochote, hata chama cha michezo tu, lazima kiendeshwe na mashabiki kwa njia za kujitolea. Moyo wa kujitolea ukifa, chama hakiwi chama tena; kinakuwa ni chaka tu la mawindo ya kujitafutia mali.”

Maneno haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

KAULI ZA WASOMAJI

Polisi iwakamate waliomuua Barlow

Ili Jeshi la Polisi liweze kujijengea hesima katika jamii, lioneshe makali yake katika kushughulikia mtandao wa mauaji ya RPC Liberatus Barlow, kufuatia maelezo yaliyotolewa na Malele.

Boniface Nyerere, Dar

Bila uwajibikaji Tanzania tutakwama (1)

Baada ya kusoma mengi katika magazeti na kuona kwenye runinga namna lile jengo la ghorofa 16 lilivyoporomoka, mimi, huenda na wengine wengi. tumeingiwa na wasiwasi.

Wabunge wa CCM wameshindwa kazi?

Sina sababu yoyote ya kuwavunjia heshima wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Lakini katika enzi hizi za ukweli na uwazi sioni, sababu ya kusita kuzungumzia masuala nyeti kwa ukweli na uwazi. Lengo langu ni kuwaomba waone ugumu wa uchaguzi wa mwaka 2015.

NUKUU ZA WIKI

Nyerere: Chama kisilazimishe watu kukichangia fedha

“Kwamwe chama [cha siasa] kisitoze kodi, au ushuru, au malipo ya nguvu-nguvu kwa mtu yeyote, awe mwanachama au si mwanachama. Michango yoyote ya fedha inayotolewa kwa ajili ya shughuli za chama lazima itokane na ridhaa ya mtoaji mwenyewe.”

Haya ni maneno ya Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

WACHONGA VINYAGO MWENGE:

Hazina ya sanaa, utalii, utamaduni isiyovuma

*Wapo wanaoongozwa na mawingu kuchonga mashetani

*Wamarekani wapendelea ‘mashetani’, Waingereza ‘wanyama’

*Baadhi watumia ‘calculator’ kuwasiliana na wateja Wazungu

*Walilia soko la uhakika, waishutumu Serikali kuwapa kisogo

Umewahi kuzuru kituo cha wachongaji na wauzaji vinyago cha Mwenge, jijini Dar es Salaam? Kama bado, basi fanya hima ufike ujionee hazina ya sanaa, utalii na utamaduni wa Kitanzania iliyotamalaki, ingawa haivumi.