JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

JAMHURI YA WAUNGWANA

Wakati mwingine Wakristo
wanaanzisha chokochoko

Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) imewasilisha mapendekezo, ikitaka kubadilishwa kwa siku ya kupiga kura ya maoni kutoka siku ya ibada – Jumapili. Mapendekezo ya CCT yamewasilishwa kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala. Mwakilishi wa CCT, Mchungaji Lazaro Rohho, anasema mabadiliko hayo yanatakiwa kuwekwa kwenye muswada wa kura ya maoni unaotarajiwa kuwasilishwa katika kikao kijacho cha Bunge.

Serikali imejipanga kuiangusha CCM

Kama tujuavyo, Serikali ya leo ya Tanzania ni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ni sawa na kusema kwamba Serikali ni mtoto wa CCM.

FIKRA YA HEKIMA

Tindikali imetuchafua,  kauli za polisi ni zilezile

Wiki iliyopita, nchi yetu ilipata doa lenye taswira ya kuichafua mbele ya uso wa Dunia. Raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) walikumbwa na mkasa wa kumwagiwa tindikali huko Mji Mkongwe, Zanzibar.

KAULI ZA WASOMAJI

CCM Rukwa tunataka serikali tatu

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Rukwa wamekwenda kinyume na msimamo wa chama chao na kutaka uwepo wa serikali tatu maana katiba ni kwa maslahi ya Taifa na sio wana CCM.

MPOROGOMYI:

Waziri mstaafu aliyeanzisha kanisa

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Dk. Kilontsi Mporogomyi, ameanzisha kanisa. Kanisa hilo lenye Makao Makuu Makongo, linatambulika kwa Jina la Kanisa la Miujiza, Uponyaji, Kufunguliwa na Mafanikio.

FASIHI FASAHA

Miaka 50 hakuna maendeleo! -3

Katika makala mbili zilizotangulia nimeandika kuhusu kichwa cha habari hapo juu. Kwa maana kuwa baadhi ya viongozi na wananchi wa kawaida wanathubutu, tena bila haya, kupiga la mgambo kuwa eti miaka 50 hakuna maendeleo huku wanaendelea kuhamisha na kuiba mali na rasilimali za nchi kama kuwa ni haki yao na kupeleka nchi za nje.