Category: Siasa
Tangu lini wapinzani wanawapenda wananchi?
Vyama vya upinzani vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) katika Bunge Maalum la Katiba vimesusia vikao vya bunge hilo tangu Aprili 16, mwaka huu.
Wapinzani wametoa sababu zao za kuchukua hatua hiyo. Kwa mfano, wamesema Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, wametoa vitisho kwamba kukiwapo Serikali tatu Jeshi litachukua nchi.
Vituko vya DC Geita vyaongezeka – 3
DC adaiwa kumtisha Roboyanke
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyara, Makoye Roboyanke (CCM), ambaye inadaiwa alivuliwa madaraka hayo na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie, amedai kuwa Septemba 10, 2013 mchana akiwa shambani kwake kijijini hapo, alipokea simu ya vitisho kutoka kwa kiongozi huyo wa Serikali.
“Alijitambulisha kwa jina moja la Mangochie na kwamba ndiye Mkuu wa Wilaya ya Geita, akaniuliza jina langu nami nikamjibu… akaniuliza ninachofanya kwa wakati huo na kazi yangu hasa ni nini, nikamwomba arekebishe kauli, na baada ya kurekebisha kauli na kuniuliza maswali ya msingi nilimpa ushirikiano.
KAGAME NI MTIHANI
Viongozi Maziwa Makuu waufanye kwa Uangalifu – 4
Tangu Kagame na RPF waitwae Rwanda ni wazi kuwa nchi hiyo inapokea fadhila za Washington DC kuliko nchi yoyote nyingine katika Maziwa Makuu.
Misaada ambayo inatoka Marekani na Uingereza kuelekezwa Kigali ni mingi na ya aina mbalimbali. Kwa hesabu rahisi misaada hiyo inafafanua ustawi wa uchumi wa Rwanda tunaouona leo.
JWTZ: Tunavifyeka vikundi vya waasi Congo
Baada ya ushindi dhidi ya Waasi wa March 23 (M23), Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na Majeshi ya Umoja wa Mataifa (MUNUSCO) limesema hakuna kikwazo chochote cha kuwaondoa waasi wa ADF- NALU na FDRL.
Ilikosewa kuruhusu UKAWA bungeni
Wiki iliyopita wanachama wa unaotajwa kuwa ni Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) walisusia kushiriki vikao vya Bunge Maalum la Katiba vinavyoendelea mjini Dodoma.
UKAWA hiyo inaundwa na wanachama wa vyama vya upinzani miongoni mwa wajumbe wanaounda bunge hilo lililokabidhiwa jukumu nyeti la kuwezesha upatikanaji wa Katiba bora ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mkurugenzi Bandari anahujumu Bodi
Uchunguzi uliofanywa na gazeti JAMHURI umebaini taarifa nyingi za uonevu katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA). Uonevu na ubabe wa Mkurugenzi, Madeni Kipande, haukuishia kwa wafanyakazi pekee, bali anaburuza hadi wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi.
Hali hii inahujumu uchumi wa nchi. Baada ya kuona hatari inayolinyemelea Taifa, mmoja wa wakurugenzi aliamua kuwasilisha hoja ya kumuondoa Kipande madarakani, lakini kwa bahati mbaya kutokana na mizizi mizito aliyonayo Kipande, wenzake watano ndiyo walioondolewa kwenye Bodi, kwa Waziri Dk. Harrison Mwakyembe kuvunja Bodi hiyo na kuteua wateule awapendao. Ifuatayo ni taarifa husika katika tafsiri isiyo rasmi. Endelea….