JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Wamiliki mabasi wana wajibu wa kupunguza ajali

Tatizo la ajali za barabarani limekuwa ni moja ya changamoto kubwa sana katika sekta ya usafiri wa barabara hapa nchini. Katika kipindi cha mwanzo wa mwezi Septemba, 2014 kumetokea ajali za barabarni kubwa zaidi ya mbili katika mikoa ya Mara na Tabora, ambako watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa.

Ukweli kuhusu elimu ya Lembeli

Mwalimu Julius Nyerere, ambaye Mheshimiwa James Lembeli amewahi kujifananisha naye, aliwahi kusema kuwa ikitokea mtu wa kawaida akampiga mkewe hadharani, hii haiwezi kuwashughulisha watu na wala haiwezi kuwa habari. Lakini ikatokea yeye (Mwalimu) akafanya hivyo, basi hiyo itakuwa habari kubwa mno.

Mwalimu Nyerere na mgombea binafsi

Mei Mosi, 1995 Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, akiwa mgeni rasmi kwenye Sherehe za Mei Mosi mjini Mbeya, alizungumza mambo mengi yaliyolihusu Taifa. Miongoni mwa mambo hayo ni haki ya kuwapo mgombea binafsi. Rasimu ya Katiba Mpya (ya Jaji Warioba) ilizingatia jambo hili muhimu. Hata hivyo, Bunge Maalum la Katiba (katika Rasimu ya Samuel Sitta) limeminya mno haki ya kuwapo mgombea binafsi. Ilivyo ni kama haki hiyo haipo kwani imewekewa vizingiti vizito mno. Soma maneno haya ya Mwalimu Nyerere.

Rais nje ya nchi kwa nusu mwezi!

Wiki iliyopita nilikuwa mkoani Mara. Nilifika katika Kijiji cha Sabasaba wilayani Butiama, mahali ambako roho takribani 40 za Watanzania zilipotea katika ajali iliyohusisha magari matatu — mawili yakiwa mabasi ya abiria yanayofanya safari zake kati ya miji ya Sirari, Musoma na Mwanza.

Sababu za Italia kusuasua kiuchumi

Licha ya dunia kuwa na jumuiya nyingi za kisiasa na kiuchumi, Umoja wa Ulaya (EU) ni kati ya jumuiya za kisiasa na kiuchumi zilizofanikiwa kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na jumuia nyingine duniani.

Ni jumuiya inayounganisha watu zaidi ya milioni 500 kutoka mataifa wanachama ishirini na nane huku pato la jumuiya likitajwa kufikia dola trilioni 18.45.

Ngeleja; Kichwa kilichojificha nyuma ya tambo za Kikwete

“Natamani kuwa Rais wa mwisho wa Tanzania kuongoza nchi ambayo ni maskini…Nimeongoza nchi maskini, lakini nataka mrithi wangu kuongoza nchi yenye ustawi na utajiri” yalikuwa ni maneno ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa Agosti 5, 2014 alipozungumza kwenye Kituo cha Kimataifa cha Maendeleo mjini Washington, D.C., Marekani.