JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Bosi TBS hachomoki

*CAG aanika madudu mengine mapya
*Omo, Blueband, mafuta ya ndege hatari
*Pikipiki feki, vinywaji hatari kwa walaji
*Aruhusu Kobil wachakachue mafuta

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ametoa taarifa ya ukaguzi maalumu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), na kuibua mambo ya hatari zikiwamo kampuni za mawaziri zinazoingiza mafuta ya magari yasiyofaa.

Wakubwa wanavyotafuna nchi

[caption id="attachment_27" align="alignleft" width="314"]Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utoah, akiwasilisha ripoti ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha wa 2009/2010 kwa waandishi wa habari bungeni mjini Dodoma, wiki iliyopita[/caption]*Kampuni ya Mohamed Enterprises yauziwa viwanja kinyemela
*Bandari watumbua zaidi ya bilioni 1.5, waendesha miradi hewa
*Mabosi wanachomeka watumishi hewa, wanavuta mishahara

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ya mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2011; imeendelea kufichua namna kundi la watumishi wa umma na wafanyabiashara wakubwa wanavyoitafuna Tanzania. Utouh aliwasilisha taarifa hiyo bungeni mwishoni mwa wiki.

Ni vita ya rushwa, haki

Uchaguzi wabunge EALA…

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano leo wanatarajia kuchangua wabunge tisa watakaoiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

CCM hofu tupu

[caption id="attachment_24" align="alignleft" width="267"]Rais Jakaya KikweteRais Jakaya Kikwete[/caption]Mwenyekiti Mkoa atoboa siri nzito
Wakati kukiwa na dalili za kuwapo uchaguzi mdogo Jimbo la Arusha Mjini, hali ya mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imeelezwa kuwa mbaya.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo ole Nangole, ameonyesha wasiwasi wake juu ya kukosekana kwa mshikamano na umoja ndani ya chama hicho kikongwe.

Wanaomiliki nyara za Serikali kukiona

Katika kukabiliana na wimbi la ujangili, Wizara ya Maliasili na Utalii imewataka watu wote wanaomiliki nyara za Serikali bila vibali, kujitokeza kueleza namna walivyozipata.

Rais Jakaya Kikwete aahidi Katiba mpya 2014

Rais Jakaya Kikwete amesema Watanzania watakuwa na Katiba mpya ifikapo mwaka 2014. Alipoulizwa kama hilo litawezekana hasa ikizingatiwa kuwa Kenya iliwachukua miaka saba kuwa na Katiba mpya, alijibu kwa mkato, “Hao ni Kenya, sisi ni Tanzania.”