Category: Siasa
RIPOTI MAALUMU
Chadema inakufa
*Mbowe, Dk. Slaa, Zitto, Shibuda hawapikiki pamoja
*Mabere Marando awatuhumu CCM, Usalama wa Taifa
*Heche, Waitara, Shonza kila mmoja lwake
*Kinana atema cheche, aeleza anachokifanya
Hali ya kisiasa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ni mbaya na tayari kumeanza kuwapo hofu ya chama hicho kikuu cha upinzani hapa nchini, kufa.
Hofu hiyo inayokana, pamoja na mambo mengine, kuibuka kwa makundi yanayohasimiana, yanayoundwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa chama hicho.
Wadau wapewa changamoto kuhusu uchimbaji uranium
Waandishi wa habari na wadau wengine wamepewa changamoto ya kuishawishi Serikali kuangalia uwezekano wa kusitisha uchimbaji wa madini ya uranium na mwingineo usiozingatia ulinzi wa afya za binadamu nchini.
NSSF: Fao la kujitoa ni hatari
*Wananchi, Serikali wahadharishwa
*Machafuko ya kiuchumi yatatokea
*Yasema ikiamuriwa ina fedha za kulipa
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) halijachoka kuwaasa Watanzania na Serikali juu ya athari za kutekelezwa kisheria kwa fao la kujitoa.
Dar es Salaam mpya
*NSSF kuanzisha miradi mikubwa jijini
*Mizigo bandarini kuondolewa kwa treni tano
*Mwisho wa malori kuingia jijini wawadia
*Nyumba zote Manzese, Vingungu kuvunjwa
Sura ya Jiji la Dar es Salaam itabadilishwa na kugeuka jiji la kisasa ndani ya miaka minne ijayo kutokana na mpango mzito ulioandaliwa na Mfuko wa Hifadhi za Jamii (NSSF).
…Mnyika: Chadema ngoma nzito
*Asema Chadema ina baraka za Mwalimu Nyerere
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetamba kwamba nguvu yake haitamalizwa na ziara za viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mikoani, katika kipindi hiki ambacho Watanzania wengi wanahitaji mabadiliko.
JK kikwazo CCM
*Yabainika ndiye mwasisi wa makundi CCM
*Akemea dhambi iliyomwingiza madarakani
Staili ya uongozi wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete, inatajwa kwamba haitakuwa na msaada mkubwa wa kuiwezesha Sekretarieti mpya kutekeleza ahadi na maazimio ya Mkutano Mkuu wa Nane uliomalizika mjini Dodoma hivi karibuni.