JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Chadema Vs Spika

*Watangaza mkakati wa kumtoa jasho katika Bunge la Bajeti linaloanza leo

*Tundu Lissu: Hatutakubali kuzibwa midomo, asisitiza yeye, wenzake hawatahojiwa

*Ndugai: Sitarajii kuona fujo zinajirudia, Shibuda kutinga na hoja ya kuahirisha bajeti

 

Wakati Bunge la Bajeti linaanza leo mjini Dodoma, wabunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wametamba kuwa kipindi hiki kiti cha Spika kitatambua makali yao.

Ridhiwani Kikwete aanika utajiri wake

*Aeleza adha za kuwa mtoto wa Rais, ataja fedha alizonazo benki

*Azungumzia urais 2015, uhusiano wake na Membe, Lowassa

*Achambua mgogoro wake na Hussein Bashe, Dk. Wilbrod Slaa

Mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani Kikwete, amefanya mahojiano maalum na Gazeti la JAMHURI nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam, Machi 30, mwaka huu, na kuzungumzia masuala mbalimbali yanayomhusu yeye binafsi na mengine yanayolihusu Taifa.

Arusha yazizima

Vifo visivyotarajiwa vya wafanyabiashara maarufu wawili – Henry Nyiti na Nyaga Mawalla – vimeibua hisia tofauti miongoni mwa wakazi wa Arusha na mikoa ya kaskazini kwa jumla. Nyiti alikuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni iliyojihusisha na uchimbaji na uuzaji vifaa vya madini ya Interstate Mining and Mineral,s iliyokuwa na makazi yake mkoani Arusha.

Lwakatare alivyorekodiwa

Taratibu mambo yameanza kuwekwa hadharani, na sasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinasema Mkurugenzi wao wa Idara ya Ulinzi, Wilfred Lwakatare, alirekodiwa na msaidizi wake, Joseph Ludovick. Hata hivyo, wakati Chadema wakiibua hayo, wanasema wanao ushahidi mzito unaonesha kuwa Ludovick alirubuniwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mwigulu Nchemba, kufanya uharamia huo.

Lowassa ajiimarisha bungeni

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa amezidi kujiimarisha kisiasa baada ya kuongeza idadi ya wenyeviti wa Kamati za Kisekta za Bunge wanaomuunga mkono.

Kibanda alivyotekwa

Mfanyakazi wa Kampuni Ikolo Investiment Ltd, Joseph Ludovick (31), aliyekamatwa na Polisi akihusishwa kwenye sakata la utekaji na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, anatajwa kuwa ni mtu muhimu katika upelelezi wa tukio hilo.