JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

BAADA YA KUANIKA MADUDU…

Ofisi ya CAG sasa yasambaratishwa

 

*Naibu CAG aondolewa, Utouh atakiwa ajiandae kung’atuka

 

Hasira za watendaji kadhaa wa Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Mashirika ya Umma na taasisi mbalimbali dhidi ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, zimeanza kuzaa matunda baada ya kuwapo mpango wa kuwang’oa viongozi wake wakuu.

India yakubaliwa kuchimba dhahabu, almasi Tanzania

 

Serikali ya Tanzania imekubali ombi la Serikali ya India, la kutaka kuwekeza katika sekta ya nishati na madini nchini.

Udokozi bandarini ukomeshwe

Bandari ya Dar es Salaam ni mashuhuri katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. Bandari hii, kwa muda mrefu, imekuwa kitovu cha biashara kati ya Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na Kati zisizokuwa na bandari (land locked).

Kwimba walilia maji safi

Mbunge wa Kwimba, Shanif Hirani Mansoor (CCM), amesema ameshaanza kushughulikia ujenzi wa mabwawa ya maji katika kata kadhaa jimboni humo.

Mchele wakosa soko Same

 

Wakulima wa mpunga wilayani Same mkoani Kilimanjaro, wameeleza kushangazwa na uamuzi wa Serikali kuruhusu uagizaji wa mchele kutoka nje ya nchi, wakati wao wamekosa wanunuzi wa tani 15,000 za bidhaa hiyo hapa nchini.

Ridhiwani Kikwete atoa ya moyoni

Wiki iliyopita gazeti hili lilichapisha sehemu ya kwanza ya mahojiano kati ya Ridhiwani Kikwete (pichani) na JAMHURI. Leo tunakulete sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano hayo.

JAMHURI: Mitandao ya kijamii unaisoma? Unajisikiaje wewe na Mheshimiwa Kikwete mnavyoshambuliwa?


RIDHIWANI: Hivi vitu kwanza tumshukuru Mungu kwa sababu Mungu amewapa watu nafasi ya kusema. Mitandao hii inatoa nafasi ya kuwafanya watu watoe yaliyomo moyoni mwao. Taarifa iliyosomwa na Waziri Mkuu mwaka 2007 ilionesha CCM ilikuwa imefanikiwa kutekeleza asilimia 98 ya Ilani ya Uchaguzi. Kufikia mwaka 2009 ikawa imetekelezwa kwa asilimia 100.