Category: Siasa
Tuhuma za ujangili: Mtutura awashukia wabaya wake, Kamanda Tossi
Wiki mbili zilizopita, Gazeti hili liliandika habari zinazohusu kukamatwa kwa msaidizi wa Mbunge wa Tunduru Kusini, Mtutura Mtutura, akiwa na bunduki za mbunge huyo zinazohusishwa kwenye matukio ya ujangili. Baada ya taarifa hiyo, Mtutura amejitokeza kukiri kukamatwa kwa bunduki hizo na ukweli wa mambo ulivyokuwa. Ifuatayo ni kauli ya mbunge huyo tunayoichapisha bila kuihariri.
Polisi matatani tena
JESHI la Polisi limeingia matatani kwa kumtangaza ‘mbaya wao’ aliyeibua kile alichodai kwamba ni mtandao wa uhalifu na mauaji ndani ya Jeshi hilo mkoani Mwanza, kwamba ni kichaa.
Mauaji ya Barlow wingu zito latanda
*Polisi wasema kijana aliyetaja mtandao ni mgonjwa wa akili
*Yeye asisitiza kuwa kichaa, analazimishwa dawa Muhimbili
*Ndugu waeleza historia, daktari anayemtibu aingia mitini
Jeshi la Polisi nchini limempeleka na kumlaza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kijana Mohamed Malele, mshirika wa mtandao uliohusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, wakidai ni mgonjwa wa akili.
RPC ‘atumika’ kuchangisha rushwa
* Watendaji wadaiwa kutumia jina lake kula rushwa kwa walima bangi
* RPC Tarime/Rorya awaruka, DC asema dawa yao inachemka
Maofisa watendaji wa Kijiji cha Kwisarara na Kata ya Bumera wanatuhumiwa kutumia jina la Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) wa Kipolisi Tarime/Rorya kuchukua rushwa ya fedha kutoka kwa wakulima wa zao haramu la bangi.
Diwani awaangukia wezi wa sola
Diwani wa kata ya Kisaka wilayani Serengeti, Chacha Togoche, ‘amewangukia’ wezi akiwaomba kutorudia kuiba sola katika zahanati ya kijiji cha Nyiboko.
Serikali yamkaanga raia wa Uswiss
. Yamnyang’anya umiliki wa ardhi aliyojipatia kinyemela
. Aliitumia kuuza viwanja kwa wageni kinyume cha sheria
. Raia wa Zimbabwe alishauziwa na kujenya nyumba
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imemnyang’anya raia wa Uswiss umiliki wa ardhi mkoani Tanga.