JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Pinda agongana na bilionea Dar

*Ni Ally Awadh wa kampuni ya mafuta ya Lake Oil
*Atuhumiwa kumfanyia unyama mtumishi wake
*Polisi Oysterbay, Kanda Maalumu wamgwaya

[caption id="attachment_1591" align="alignleft"]Mlalamikaji anayedaiwa kupigwa na mabaunsa wa mfanyabiashara bilionea Ally Awadh (Lake Oil)[/caption]Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ameamua “kujipima uzito” dhidi ya bilionea Mtanzania, Ally Edha Awadh ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Lake Oil ya Mikocheni jijini Dar es Salaam inayoagiza, kuuza na kusafirisha mafuta na biashara nyingine nyingi.

Awadh anayetajwa kama mmoja wa mabilionea vijana nchini, amefunguliwa mashitaka Polisi ya kumteka, kumdhalilisha kinyume cha maumbile na kumpora mali mmoja wa wafanyakazi wake.

Uamuzi wa Waziri Mkuu Pinda umekuja baada ya Jeshi la Polisi nchini, katika kile kinachoonekana ni kumgwaya bilionea huyo, kupuuza kumsaidia mlalamikaji huyo mwenye umri wa miaka 32. Kwa sababu za kiutu na za kitaaluma, jina la mlalamikaji tunalihifadhi kwa sasa.

Kitanzi cha JK

Wizara ya Maliasili yatajwa kuwa mtego kwa Kikwete

Pinda, Mwamunyange, Mwema watakiwa kupima uzito

Rais Jakaya Kikwete, akiwa anatarajiwa kulisuka upya Baraza la Mawaziri, kuna kila dalili kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa sasa ndio imebaki kuwa kitanzi kinachotishia uhai wa Serikali yake.

Siri ya Mandela

*Alisahau viatu vyake vya kijeshi Tanzania, akafungwa

*Mufti Simba, Askofu Kilaini, Ruwa’ichi watoa tamko

*Profesa Baregu, Wangwe, Safari, Kiwanuka wanena

 

Kifo cha Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela “Madiba”, kimefichua siri nzito kuhusu harakati zake za ukombozi wa taifa hilo kutoka katika makucha ya serikali ya kibaguzi ya Wazungu.

M23 yawafika mazito

*UN waanza kutumia ndege zisizo na rubani kusaka masalia

*Zinatambua aliko mwenye bunduki, zilitumika Afghanistan

 

Baada ya Brigade Maalum ya Umoja wa Mataifa ikiongozwa na Jenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuwasambaratisha waasi wa M23 nchini DRC, Brigade hiyo imeanza kutumia ndege zisizokuwa na marubani (drones) kufanya ulinzi katika mji wa Goma, hali inayozidi kuwafukizia moshi waasi hao.

Jahazi Asilia: CCM, CUF wanahofu vivuli vyao

Chama cha Jahazi Asilia kimesema mtindo unaotumiwa na vyama vya CCM na CUF kubeba wanachama kwenda na kurudi kwenye mikutano ya hadhara hauvikisaidii vyama hivyo kujitambua na kupima kisiasa kama vinakubalika au la.

M23 walia njaa

Waona giza nene mbele yao, Uganda yaonya vita inanukia
DRC yazidisha mashaka kwa Uganda, Watanzania waonya

Hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kukataa kusaini mkataba wa amani na kundi la waasi la M23, imepeleka kilio kwa kundi hilo, na sasa wanalia njaa uhamishoni nchini Uganda.