JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

MAGHALA TANDAHIMBA: Vigogo wamfuata Waziri Chiza

Kampuni ya Tandahimba Quality Control System, iliyoshinda kwa utata zabuni ya kuendesha maghala ya Muungano wa Vyama vya Ushirika Wilaya za Tandahimba na Newala (TANECU), inahaha ngazi za juu ili ikabidhiwe maghala hayo.

Kampuni hiyo inatafuta njia za mkato, ikiwezekana kwa kumtumia Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, ili ikabidhiwe shughuli hiyo yenye ukwasi mkubwa.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Leseni za Maghala, Fidelis Temu, ameiandikia Tandahimba Quality Control System barua ili ijibu hoja za pingamizi zilizotolewa na wadau kadhaa kwa maandishi.

Al-Shaabab, Boko Haram waungana

KUNDI la kigaidi la Al-Shabaab la nchini Somalia ko kwenye wakati mgumu kama Boko Haram la Nigeria ambalo taarifa za kuuawa kwa kiongozi wake, Abubakar Shekau.

Kutokana na hali hiyo, taarifa zinasema kwamba kumekuwa na mawasiliano baina ya makundi ya kigaidi kuunganisha nguvu za pamoja ili kukabiliana na hali ya kuzidiwa na wapinzani wao katika harakati zao.

JK amchoka Nyalandu

*Atinga Marekani na msanii wa ‘Bongo Movie’

*Wabunge wamsubiri kumsulubu Novemba

*Safari, hoteli ghali zatafuna mamilioni ya shilingi

*Ofisi zake za wizarani ‘zakaribia kuota majani’

 

Na Mwandishi Wetu

 

Rais Jakaya Kikwete ameanza kuchoshwa na vituko vya Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, JAMHURI limethibitishiwa.

Wataalamu: Mtoto mpotevu Dar ana tatizo la kisaikolojia

Wanataaluma nchini wamesema kwamba wamefuatilia habari za kupotea na kupatikana kwa mtoto Happy Rioba (9), na kwa haraka wamegundua kwamba binti huyo ana tatizo la saikolojia tofauti na wengi wanaohusisha ushirikina.

Happy, anayeishi na mama yake, Sarah Zefania huko Mkuranga mkoani Pwani, aliripotiwa na vyombo vya habari kupotea na kupatikana zaidi ya mara moja, tukio lililovuta hisia za watu wengi.

Kwa mtego huu wa UKAWA hautamnasa Rais Kikwete

Tukio la hivi karibuni ambapo wajumbe wanaounda kundi la Umoja wa Katiba wa Wananchi (UKAWA) kuamua kuyakana makubaliano yaliyofikiwa baina yao na Rais Kikwete kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), haliwezi kupita bila kuhojiwa.

Mbowe moto

.Adai moto aliowasha hauzimiki mpaka kieleweke 2015

.Asema anaumizwa kuteketea mamilioni Bunge la Katiba

.Atamba ipo siku polisi watazitambua haki za Watanzania

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema anashangazwa na vigogo wa Jeshi la Polisi kufanya hila za kumkabili, ilhali wanaona namna Watanzania walivyodhulumiwa haki yao kupitia Bunge Maalum la Katiba.