JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Putin anakuja Tanzania

LICHA ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kusuasua kuthibitisha kuhusu ujio wa Rais wa Russia, Vladimir Putin taarifa za uhakika zinasema kwamba mwamba huyo wa kimataifa atatua nchini Februari, mwakani.

Obama anataka niwe Rais Tanzania-Waziri

*Wabunge wakataa ‘hongo’ ya safari ughaibuni aliyowaahidi

*Ripoti aliyowasilisha yatupwa, wasema imejaa ubabaishaji

*Msanii aliyekuwa Marekani na Nyalandu, Aunty Ezekiel anena

Waziri aonya rushwa Zimamoto

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima, amewataka askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuepuka tamaa hasa vitendo vya kupokea rushwa.

Kibao chawageukia Al-Shabaab, Boko Haram

INTELIJENSIA ya Serikali za Nigeria na Somalia, zimeshtukia mipango ya makundi ya kigaidi ya Al-Shaabab na Boko Haram yaliyopanga kuungana, lakini mambo yamewawia ugumu.

Aunty Ezekiel atanua na Nyalandu Marekani

*Ni msanii aliyedokezwa na gazeti hili wiki iliyopita

*Mrembo akiri walikuwa pamoja kutangaza utalii

*Asisitiza sehemu kubwa ya bajeti ilitoka wizarani

*Yaelezwa ndicho kilichomkera Rais Kikwete Marekani

Ni ufisadi wa kutisha Geita

Viongozi wa kijiji wajichotea fedha ‘kiulaini’

 

Vigogo watatu wa Kijiji cha Mawemeru kilichopo katika Kata ya Nyarugusu, Wilaya ya Geita, mkoani hapa wanatuhumiwa kujigeuza “Miungu-watu” kwa kutafuna fedha za wanakijiji Sh 50 milioni.

Kwa nafasi hiyo, vigogo hao wanadaiwa kukigeuza kijiji hicho “shamba la bibi” huku wananchi wanaojitokeza kuhoji taarifa ya mapato na matumizi wakitishwa na wengine wakiishia kuswekwa ndani.

Vigogo waliokumbwa na tuhuma hizo ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji, Agness Matibu, Mwenyekiti wa Kijiji, Mussa Maduhu, pamoja na Mchumi, Philipo Kamuye, ambao, kwa kushirikiana wanadaiwa kutafuna kiasi hicho cha fedha.

Fedha hizo, zaidi ya Sh 50 milioni zinatokana na vyanzo vya ndani vya mapato yatokanayo na kijiji. Kadhalika sehemu ya fedha hizo hutokana na mapato yatokanayo na wawekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi.

Vyanzo vya gazeti hili vilidai kuwa vigogo hao kwa pamoja wameshirikiana kufisadi mapato ya kijiji na kwamba suala lolote linalohusu fedha zitokanazo na vyanzo hivyo, hakuna mwananchi anayeruhusiwa kuhoji na hawajawahi kusomewa taarifa za mapato na matumizi tangu mwaka 2011.