Category: MCHANGANYIKO
Mwanasheria Mkuu awamaliza Uamsho
*Asema wanataka kuipeleka Zanzibar vichakani
Mchakato wa kuandika Katiba Mpya umepata hamasa kubwa hasa visiwani Zanzibar. Huko kuna kundi la dini lijulikanalo kama Uamsho. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman, ameamua kuweka mambo sawa kwa kile anachoona jinsi kikundi cha Uamsho kinavyoipotosha jamii. Endelea…
Mkaa ni janga la kitaifa
Nimemsikia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, aliihoji Serikali ili ieleze mipango ya haraka ya kuokoa theluji katika Mlima Kilimanjaro.
Waislamu wapuuzeni kina Ponda
Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limetangaza rasmi kutoshiriki sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti, mwaka huu.
Maradona, toka Mwanasoka Bora wa Dunia hadi teja la mihadarati
ALIZALIWA Oktoba 30, 1960 katika jiji la Buenos Aires, Argentina, kutokana na ndoa ya Diego Maradona na mkewe, Dalma Salvadore ambapo pia naye akaitwa Diego Maradona, kisha akatokea kuwa mwanasoka aliyetamba duniani.
Mwenyekiti aparaganisha halmashauri Karagwe
*Adaiwa kuchota 270,000, yeye ajibu hoja zote
Halmashauri Wilaya ya Karagwe imeingia katika mgogoro mpya, baada ya madiwani na watendaji wengine kuanzisha harakati za kumg’oa Mwenyekiti wa Halmashauri, Kashunju Singsbert Runyogote, ambaye naye amejibu mapigo kwa kuzima harakati hizo.
Yah: Saba Saba na vinyozi na wapigadebe tunakwenda wapi?
Wanangu, nawashukuruni kwa kusoma mambo ya zamani pamoja na kwamba yanawakera, kwa sababu wengi wenu mnaona kama historia na ambayo labda mengine hayakuwahi kuwaingia vichwani kwamba yaliwezekana na yalitekelezeka.
Niliwahi kuwaandikia barua hii kuwakumbusha juu ya barua ambazo tulikuwa tukiandika, na ilichukua mwezi au zaidi kumfikia aliyeandikiwa. Barua hiyo ilikuwa na ujumbe mzito haiyumkiniki zilikuwa habari za uzazi, ndoa, vifo, majanga na hata tukio la furaha kijijini kwetu.
Baada ya miaka kadhaa ya Uhuru tulianzisha Shirika la Posta na Simu ambalo wakati huo simu zote zilikuwa zikiunganishwa Dodoma kwenda katika mikoa mingine. Hii ilikuwa njia ya haraka sana ya mawasiliano, lakini haikuwa kwa watu wote, bali wachache tu waliochukulia jambo lao ni la haraka sana.